Home » » MAGEMA KUPELEKA KILIO CHAO KWA PINDA

MAGEMA KUPELEKA KILIO CHAO KWA PINDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Waziri Mkuu, Mizengo PindaBAADA ya uongozi wa Wilaya na Mkoa wa Geita kukaidi kusikiliza malalamiko ya wananchi wa Kitongoji cha Magema kilichopo kijiji cha Nyamalembo, wananchi hao wameazimia kupeleka malalamiko yao kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ili kupatiwa ufumbuzi.
Wakizunguza katika mkutano wa pamoja juzi, ambao ulijadilia mstakabali wa maisha yao tangu serikali kupitia kwa Mkuu wa Wilaya, Omar Mangochie kuzuia kufanya shughuli zozote katika maeneo yao, wanakijiji hao walisema kuwa uongozi wa wilaya umekuwa ukiwadhalilisha mbele ya wawekezi wa mgodi wa GGM.
Walidai kuwa wamefanya kila jitihada za kuweka mahusiano mazuri dhidi ya mwekezaji kuhusu malalamiko yao ya kutofanyiwa tathimini na kulipwa ili waweze kuondoka eneo hilo, lakini uongozi wa serikali hususan mkuu wa wilaya, umewapuuza.
Wameeleza kuwa wamefikiwa uamuzi wa kupeleka malalamiko yao kwa Waziri Mkuu kwa vile wanaimani kuwa atawatatulia matatizo yao ili waweze kurejea katika gurudumu la kuendeleza maisha yao na taifa kwa ujumla.
“Tulimwandikia barua mkuu wa wilaya, kumwomba aje katika mkutano wetu ili atusikilize matatizo yetu, lakini cha kushangaza aliita viongozi wa kata na viongozi wa mgodi wa Geita Gold Mine (GGM) na alichokifanya alitufokea na kutoa vitisho mbele ya wawekezaji hao, hivyo tumeona sasa tusonge mbele,” walidai.
Wakifafanua zaidi kuhusu sakati hilo, walisema kuwa awali walipewa amri ya kutofanya shughuli zozote za maendeleo katika maeneo hayo ikiwemo kulima na uchimbaji madini kama ilivyokuwa zamani, jambo ambalo limewasabishia umasikini na kushindwa kupata chakula, kusomesha watoto wao na mahitaji mengine.
“Sasa hivi tunalazimika kuchimba kwa kujifuchaficha ili tuwezo kuendesha maisha yetu, maana serikali imeshindwa kabisa kutujali sisi wananchi wake hata kututafutia maeneo mengine ya kuishi,” waliongeza.
Alipotakiwa na gazeti hili kutoa ufafanuzi kuhusu sakata hilo, mkuu wa wilaya, Omar Mangochie kwa njia ya simu, alikanusha vikali wananchi hao kutakiwa kuondolewa katika maeneo hayo na kwamba wamezuiwa kufanya uchimbaji wa madini kwa kuwa ni eneo la mgodi.
“Hawajaambiwa kuondoka, tulichowaambia ni kuacha shughuli za uchimbaji madini kwa kuwa ni kinyume cha sheria ya madini namba 14 ya mwaka 2010, kwa sababu kuchimba madini ni lazima uwe na leseni, lakini pia wanaharibu mazingira,” alieleza.
Hata hivyo, alisema hakumbuki kama aliandikiwa barua ya kualikwa kwenda katika mkutano huo wa wanachi uliokuwa na lengo la kujadili na kutatua matatizo yanayowakabili.
Gazeti hili linayo nakala ya barua hiyo ya Julai 5 mwaka huu, iliyoandikwa na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Magema, Leonard Kalumwa, ikimwomba mku wa wilaya ahudhirie mkutano wa wanakijiji hicho na nakala  kwenda kwa Ofisa Uslama wa wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya, Mkuu wa Polisi wilaya, Ofisa Tarafa ya Geita na Diwabni wa Kata ya Mtakuja.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa