Home » » DC MASALLA ASHAURI MAONESHO YA NANENANE YAVUTIE ENEO LA MAZIWA MAKUU

DC MASALLA ASHAURI MAONESHO YA NANENANE YAVUTIE ENEO LA MAZIWA MAKUU

Waandaaji wa maonesho ya Nanenane mikoa ya Kanda ya Ziwa Magharibi Mwanza,Geita na Kagera wameshauriwa kuzidi kuipa hamasha maonesho hayo na kuzifikia nchi zote za maziwa makuu kutokana na Mkoa wa Mwanza kuwa eneo la kimkakati.

Rai hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masalla alipotembelea baadhi ya mabanda na kujionea na kupata taarifa mbalimbali kutoka kwa washiriki na kuhimiza fursa ya Mwanza kuwa eneo la kimkakati itumike vizuri kuyapa wigo maonesho hayo.

"Mwanza siku chache zijazo itazidi kuimarika hasa katika eneo la usafiri kuanzia wa anga,reli na barabara hivyo ni wakati mwafaka kwa waandaaji kuja na ubunifu wenye sura ya kimataifa utakao leta tija ya kiuchumi.

Amesema ukanda huu wa nchi za maziwa makuu umejaa wakulima na wafugaji,na makundi mengine na katika maonesho haya kuna utoaji wa elimu ya kitaalamu namna ya kupata tija hata ukiwa na mifugo michache au kuvuna mazao bora kwa muda mfupi bila kitegemea mvua.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amewataka Taasisi mbalimbali zinazotoa huduma za Utafiti wa kilimo kwa ujumla ziongeze huduma hizo kwa wakulima wote nchini kutokana na sekta hiyo kuingiza fedha nyingi hivi sasa.

Viongozi mbalimbali wanaendelea kuyatembelea maonesho hayo yatakayo fikia tamati Agosti 8 mwaka huu.

Kauli mbiu ya maonesho hayo ni”chagua viongozi bora wa Serikali za mitaa kwa maendeleo endelevu ya kilimo,mifugo na uvuvi.”

 


0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa