MKUU WA MKOA GEITA AWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI KWENYE KAMPENI YA ELIMU KWA MLIPAKODI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

MHE BITEKO AANZA KUTEKELEZA AGIZO LA WAZIRI MKUU LA KUKOMESHA UTORO MASHULENI, ACHANGIA MATOFALI 10,000 UJENZI WA MAABARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita ambaye ni Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua majengo ya maabara za shule ya sekondari ya Kata ya Busonzo katika Kijiji cha Nampalahala akiwa katika ziara ya siku moja Wilayani Bukombe, Leo 2 Aprili 2018. Picha Na Mathias Canal-Wazo Huru Blog
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita ambaye ni Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua nyumba ya walimu katika shule ya sekondari ya Kata ya Busonzo katika Kijiji cha Nampalahala, Leo 2 Aprili 2018. 
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Nampalahala, Kata ya Busonzo wakifatilia mkutano wa hadhara ukiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita ambaye ni Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko wakati akiwa katika ziara ya siku moja Wilayani Bukombe, Leo 2 Aprili 2018.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita ambaye ni Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Nampalahala, Kata ya Busonzo wakati akiwa katika ziara ya siku moja Wilayani Bukombe, Leo 2 Aprili 2018.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita ambaye ni Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua ujenzi wa nyumba za madaktari wa kituo cha afya cha Uyovu akiwa katika ziara ya siku moja Wilayani Bukombe, Leo 2 Aprili 2018.

Na Mathias Canal, Geita

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita ambaye ni Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko Leo 2 Aprili 2018 amechangia matofali 10,000  kwa ajili ya ukamilishaji Wa vyumba vya maabara ili kurahisisha uanzisha Wa shule ya sekondari Kata ya Busonzo Wilayani Bukombe.

Shule ya sekondari Busonzo inahitaji kukamilisha maabara tatu ili iweze kufunguliwa ambapo serikali imetoa milioni 40 kwa ajili ya kazi hiyo.

Mhe Biteko amechangia matofali hayo Mara baada ya maagizo ya Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa aliyoyatoa wakati Wa dhifa ya uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2018 katika uwanja wa Magogo mkoani Geita kwa kuwataka viongozi wa mikoa ya Tabora, Geita, Mtwara na Shinyanga ambayo inaongoza kwa utoro wa wanafunzi kwa shule za msingi na kwa sekondari wahamasishe umuhimu wa elimu na mahudhurio endelevu shuleni.

"Mkoa wetu tumepata aibu kubwa kwa kuwa namba mbili kwa utoro kati ya mikoa yote nchini, utoro huu hapa wilayani kwetu unachangiwa na umbali wa kwenda shuleni, hapa Busonzo watoto wetu wanasoma Runzewe ambapo ni mbali sana. Umbali huo unachangia utoro" alisisitiza Mhe. Biteko

Katika sherehe hizo zilizonakshiwa na Kaulimbiu ya mbio za mwenge kwa mwaka huu ambayo ni ‘Elimu ni ufunguo wa maisha, wekeza sasa kwa maendeleo ya Taifa letu.’ Waziri Mkuu alisema kuwa utoro wa wanafunzi wa Sekondari ni mkubwa zaidi kwa Mikoa husika kuliko shule za msingi. 

Mara baada ya uzinduzi Wa Mwenge huo wa Uhuru kabla ya kuelekea Mjini Dodoma kwa ajili ya shughuli za Bunge zinazotarajiwa kuanza kesho 3 Aprili 2018 Mhe Doto Biteko amezuru Kijiji cha Nampalahala kilichopo Kata ya Busonzo na kujionea jinsi ujenzi Wa maabara unavyoendelea.

Mara baada ya kubaini kuwa kuna upungufu wa matofali 10,000 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo, Naibu Waziri huyo amechagiza ujenzi huo kwa kuchangia gharama za ununuzi wa matofali hayo ili ujenzi huo ukamilike kwa wakati.

"Mheshimiwa Waziri Mkuu ameshatoa maelekezo ya kukomesha utoro naomba tukimbie kulitekeleza hilo na ninaomba wazazi tuhakikishe watoto wote wanakuwa shuleni ni aibu mno sisi kuwa vinara wa utoro". Aliongeza Mhe. Mbunge Na Naibu Waziri huyo.

Mhe Biteko amewaeleza wananchi hao jinsi ambavyo utoro kwa shule za sekondari Mkoani Geita umekithiri jambo ambalo limepelekea Mkoa huo kushika nafasi ya pili kwa utoro Kitaifa kwa asilimia 8.1, ambapo Mtwara imekuwa nafasi ya tatu kwa asilimia 6.4, Shinyanga asilimia 6.3 huku nafasi ya kwanza ikishikiliwa na Mkoa Wa Tabora kwa asilimia 9.7 

Aidha, Mhe Biteko ameonyesha kusikitishwa na takwimu za Mkoa Wa Geita kushika nafasi ya pili pia katika kwa utoro kwa shule za msingi kwa kwa asilimia 3.1 nyuma ya Mkoa Wa Rukwa unaoongoza kwa asilimia 3.2

Aliongeza kuwa anatamani kuona  Wilaya ya Bukombe inahakikisha inafikia viwango bora vya elimu. Serikali ya awamu ya tano inyoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli, imedhamiria kuboresha elimu katika ngazi zote nchini, kuanzia Elimu ya Awali hadi Elimu ya Juu hivyo wananchi wanapaswa kuitumia fursa hiyo kwa maendeleo ya wilaya hiyo na Taifa kwa ujumla aliwaomba pia wananchi wa  kata ya Busonzo kumuombea Rais Magufuli na kuunga mkono juhudi za serikali.

Kaya 467,609 Zapatiwa Vyandarua bure Geita DC

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399


Halmashauri ya wilaya ya Geita imefanikiwa kugawa vyandarua vyenye viuwatilifu 131,445 kwa uwiano wa  chandarua kimoja kwa watu wawili kwa jumla ya kaya  467,609 katika harakati za kutokomeza ugonjwa wa malaria ambao bado ni tishio kwa eneo la kanda ya ziwa.
Akiongea wakati wa kikao cha kutathimini hali ya malaria wilayani hapa kaimu mratibu wa malaria wilaya ya Geita ndugu Fredy Mwaipaja amesema Maambukizi ya malaria yamepungua  kutoka asilimia 16.3% mwaka 2016 hadi 15.1% mwaka 2017 kwa wagonjwa  112,134 sawa na asilimia 36.5% kati ya wagonjwa  310,251 waliofika katika zahanati na vituo vya afya ambao ni wagonjwa wa nje maarufu kama OPD .
Utafiti wa malaria uliofanyika mwezi Oktoba, 2017 katika shule 5 za Msingi  Halmashauri ya wilaya Geita unaonyesha  wanafunzi  396 kati ya 674 sawa na asilimia 58.8% ya wanafunzi waliopimwa waligundulika na vimelea vya Malaria hali iliyopelekea  Halmashauri kuja na mkakati mwingine wa kuhakikisha vyandarua vyenye viwatilifu  vinagawiwa shuleni  na pia watoto wanafundishwa mbinu mbalimbali za kupambana na Malaria.
Mwaipaja  ameeleza  kiwango cha upimaji wa malaria kimeongezeka kutoka asilimia 91.8% mwaka 2016 hadi asilimia 98.8% mwaka 2017 na watu waliogundulika  wana malaria walipatiwa tiba.
Akilezea Sababu zinazochochea maambukizi ya malaria katika jamii ni pamoja na tabia ya jamii kuchelewa kufika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kwa ajili ya utambuzi na kupata tiba ya malaria, Kutumia dawa bila kupima,  kutokamilisha dozi kwa wagonjwa wa malaria, Matumizi yasiyo rasmi ya vyandarua kwa shughuli zisizokusudiwa pamoja na  Kugomea shughuli za unyunyiziaji wa dawa ya ukoko majumbani”.
“Katika kuhakikisha Malaria inaondoka kabisa Geita kwa sasa tunatoa elimu kwa jamii na tunahakikisha matumizi salama na sahihi ya vyandarua yanatelekezwa na ndio maana tumeamua kugawa vyandarua hivyo kwenye ngazi za shule za msingi kama njia mojawapo ya kuzuia malaria” Ameongeza Mwaipaja.
Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita baina ya Wataalam kutoka Halmashauri ya wilaya ya Geita pamoja  na mashirika yasiyo ya kiserikali ya “Tanzania Communication and Development Center”(TCDC),Pamoja na New Light Children Organisation (NELICO)  kwa lengo la kutathimini hali ya Ugonjwa wa  Malaria wilayani hapa.

Geita DC yapitisha Bilioni 77.6 Mwaka wa Fedha 2018/2019

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

Na Bathromeo C Chilwa
Afisa Habari Geita DC

Baraza la madiwani Halmashauri ya wilaya ya Geita limepitisha makadirio ya bajeti ya matumizi ya mwaka wa fedha 2018/2019 kiasi cha shilingi bilioni 77,673,234,821. Ikiwa ni ongezeko la shilingi bilioni 1,173,780,082.13 sawa na asilimia 1.5 % kutoka katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 kiasi cha shilingi bilioni 76,499,454,738.87, iliyotengwa .
Katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Geita kikao cha baraza  la madiwani  kiliongozwa na Mheshimiwa Hadija Said Makamu mwenyekiti wa Baraza hilo na kuhudhuriwa na Mbunge wa jimbo la Busanda Mheshimiwa Lolensia Bukwimba, Waheshimiwa Madiwani, Wataalam wa Halmashauri, Viongozi wa vyama vya siasa na wadau wengine wa maendeleo kutoka wilayani hapa.
Katika bajeti hiyo shilingi bilioni 18,040,010,550/=  ambazo ni fedha za ruzuku zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo, Shilingi bilioni 2,440,501,771/= ni fedha za ruzuku zitakazotumika kwa matumizi ya kawaida (OC), Shilingi bilioni 53,607,008,000/= zitatumika kulipa mishahara, shilingi bilioni 3,585,714,500/=  ni makusanyo ya ndani, shilingi bilioni 1,297,941,800/= ni matumizi ya kawaida ya mapato ya ndani (OS) na Shilingi bilioni 2,084,412,700/= zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo, shilingi milioni 203,360,000/= ni matumizi ya mapato mengine ambayo ni (CHF,NHIF/User fee) na shilingi bilioni 1.5 zitakuwa ni nguvu za wananchi kuchangia miradi ya maendeleo.
Sambamba na hilo Halmashauri  imeainisha chanzo kipya cha mapato ambacho ni kituo cha redio cha rubondo kinachotarajiwa  kuanza kazi hivi karibuni kukasimiwa katika bajeti na kukadiriwa kuingiza kiasi cha shilingi milioni 250.
Bajeti hii  ina matarajio makubwa ya kuboresha huduma za jamii kupitia sekta za Elimu, Afya, Maji,Ardhi na Mifugo, Pia Kuboresha miundombinu ya ufundishaji na kufundishia mashuleni kwa kujenga shule za elimu ya juu(A’Level), Hosteli za wasichana, Vyumba vya madarasa,Nyumba za walimu, Maabara na kutoa Motisha kwa walimu kwa lengo la kuongeza ufanisi.
Source www.geitadc.go.tz

WAENDESHA BAISKELI ZA ABIRIA WAPINGA AGIZO LA KUONDOKA MJINI GEITA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Baadhi ya waendesha Baiskeli maarufu kwa jina la dala dala wakiwa wamekusanyikana sehemu moja kujadili mustakabali wa kuondolewa kwenye maeneo ya mjini.

Waendesha Baskeli wakiwa maeneo ya mjini  Geita.


Waendesha Baiskeli wakitafakali juu ya hatua ya kuondolewa mjini Geita.

Na,Joel Maduka,Geita.


Waendesha Baiskeli Maarufu kwa jina la daladala wanaosafirisha abiria kwenye halmashauri ya mji wa Geita, wamepinga agizo la Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo la kuwataka kufikia leo wasitishe shughuli zao kwenye maeneo ya mjini badala yake wafanye kwenye maeneo waliyopangiwa.

Hatua hiyo imekuja baada ya kupewa muda wa siku tano kupisha maeneo ya mjini kutokana na wimbi la ajali zinazosababishwa na waendesha Baiskeli kwa kutotumia barabara vizuri wanapokuwa kwenye shughuli zao.

Baadhi ya waendesha Baiskeli hao Bw Vistusi Maagani, John Maige na Fredy Maganga wamesema utaratibu uliofanyika sio mzuri kwa kuwa hawajapewa maeneo yatakayowasaidia kufanya kazi zao .

“Nasikitishwa sanaa na kitendo cha Mkurugenzi kututoa bila ya kutuandalia maeneo mazuri ya kufanyia kazi zetu kwa mfano mimi hapa hii kazi ndio nategemea kulisha familia pia kutuma pesa kwa mama yangu mzazi kwa kuwa sina ndugu leo natolewa kufanya kazi mjini unategemea nitaishi maisha gani jamani na wale ambao wananitegemea nitawaelezaje mimi naomba haya maamuzi wayaangalie kwa umakini”Alisema Maagini.

“Nashindwa hata niseme nini najisikia moyo wangu kutoka  kabisa kutokana na taarifa hii ya kuondolewa mjini maeneo ambayo tunaambiwa kufanya kazi akuna abiria sasa sijui tutaishije sisi waendesha daladala”Alisema  Maganga.

Bi,Lucia Paul ambaye mume wake anajishughulisha na kazi hizo alisema  kuondolewa mjini kwa waendasha baiskeli kutaleta athari kwenye familia zao kutokana na wengi wao kutegemea shughuli hiyo kukidhi mahitaji ya familia.

“Kwasasa hivi nyumbani hapakaliki kila siku mume wangu anamawazo anashindwa afanye nini na uku anafamilia muda mwingine hadi namuonea huruma  serikali ni vyema ikaangalia maana itatupa wakati mgumu sisi wanawake ambao tunawategemea waume zetu kwenye utafutaji”Alisisitiza Lucia.

Kutokana na hali hiyo chama cha ACT wazalendo kupitia kwa katibu wa mkoa huo,Bw Ikolongo Otoo  ameitaka halmashauri ya mji wa Geita kuondoa mara moja zuio hilo  kwa kuwa ni la kibaguzi ambalo alijazingatia wala kuthamini vijana masikini na wanyonge ambao wameamua kujipatia vipato kwa njia halali kabisa.

Mkurugenzi wa Halmashari ya mji wa Geita,Mhandisi Modest Aporinaly  alisema suala ambalo linafanyika ni la utekelezaji na alilikuwa aliitaji  muda kwani maeneo ambayo wamewapatia kufanya biashara ni makubwa na kwamba hata wangepewa muda  wa kutosha bado wangeombwa kuongezewa.

Mbunge wa Jimbo la Geita mjini,Constatine Kanyasu alisema  ahafikiani na makubaliano hayo na kwamba akuna utaratibu wala sheria ambayo inawazuhia waendesha Baiskeli kufanya shughulo zao maeneo ya mjini.

BALOZI WA JAPAN AKABIDHI SOKO LA KIMATAIFA LA SAMAKI KASENDA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kushoto  ni  Balozi wa Japan nchini Tanzania , Masaharu Yoshida akiwa na mkuu wa mkoa wa Geita ,Mhandisi Robert Luhumbi baada ya kukabidhi  soko la samaki la kimataifa la Kasenda  lililopo kata ya Mganza Wilayani Chato lililojengwa kwa ufadhili wa serikali ya Japan. 


Balozi wa Japan nchini Tanzania , Masaharu Yoshida akizindua kwa kuweka jiwa la msingi kwenye mradi wa soko la samaki la kimataifa la kasenda pamoja na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Chato ,Mhandisi Joel Hari.

Balozi wa Japan nchini Tanzania , Masaharu Yoshida  akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi wakati wa hafra fupi ya kukabidhi soko la kimataifa la Samaki.

Mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akibadilishana mawazo na Balozi wa Japan nchini Tanzania , Masaharu Yoshida  pamoja na mbunge wa jimbo la Chato Dk,Medard Kalemani.

Jiwe la msingi ambalo limewekwa na Balozi wa Japan nchini Tanzania , Masaharu Yoshida  kwenye soko la samaki la kimataifa la Kasenda.

Balozi wa Japan nchini Tanzania , Masaharu Yoshida akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa serikali pamoja na chama cha mapinduzi(CCM)

Balozi wa Japan nchini Tanzania , Masaharu Yoshida  akizungumza na wananchi baada ya shughuli ya kukabidhi na kuweka jiwe la msingi kwenye soko la samaki la kimataifa.

Muonekano wa soko la Samaki la Kimataifa la Kasenda Wilaya ya Chato mkoa wa Geita

Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi na Balozi wa Japan nchini Tanzania , Masaharu Yoshida  wakiweka saini kwenye vitabu vya wageni.


Na,Joel Maduka,Chato.

Balozi wa Japani nchini Tanzania Masaharu Yoshida  kwa kushirikiana na serikali ya mkoa wa Geita amezindua rasmi soko la kimataifa la uuzaji samaki la kasenda lililojengwa kata ya mganza wilayani chato mkoani hapa kwa hisani ya watu wa Japani.

Soko hilo lililopo kata ya Muganza lina jumla ya wafanyabiashara wa samaki zaidi ya 240 limegharimu jumla cha Shilingi milioni 320 za kitanzania hadi kukamilika kwake ukarabati uliohusisha pia ukarabati wa soko la zamani. 

Akikabidhi soko hilo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Balozi wa Japan nchini Tanzania mhe. Masaharu Yoshida amesema kukamilika kwa ujenzi wa ghala la kuhifadhia samaki na dagaa kutasaidia kuokoa mazao mengi kutoka ziwani hususan samaki na dagaa.

“Soko la samaki la Kasenda halikuwa na miundombinu ya kuhifadhia samaki ambapo zaidi ya tani 200 za samaki zilitupwa kila mwaka kutokana na kuharibika ambapo serikali” alisema Mhe Masaharu.

Wakati huo huo serikali ya Japan imesaini mkataba na Halmashauri ya Wilaya ya Chato ya ukarabati wa barabara kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa moja kutoka Muganza hadi Kasenda mahali lilipo soko hilo kwa thamani ya shilingi milioni 197.

Waziri wa Nishati mhe.Dkt. Medard Kalemani ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Chato ameishukuru serikali ya Japan kuendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania. Alisema serikali ya Japan kwa muda sasa imekuwa ikishirikiana na Wilaya ya Chato na hii inatokana  na uhusiano mzuri ulioanzishwa na mbunge wa Chato kwa wakati huo mhe. John Pombe Magufuli.

Mkuu wa Mkoa wa Geita mhandisi Robert Gabriel  amewataka wananchi pamoja na uongozi wa soko kushirikiana na uongozi wa Halmashauri ili kuhakikisha malengo ya uanzishwaji wa soko hilo yanatimia likiwemo suala zima la ukusanyaji wa mapato.

Mbali na kuhudumia soko la ndani ya nchi, soko hilo la kimataifa la Kasenda limekuwa likihudumia baadhi ya nchi za jirani kama vile Congo DCR, Rwanda, Burundi na Uganda.Ambapo  linakadiriwa kukusanya Zaidi ya shilingi milioni 140 kwa mwaka.

WAZIRI KALEMANI AMWASHIA MOTO MKANDARASI ANAYESAMBAZA UMEME VIJIJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Chato,Dk Medard Kalemani akitoa maagizo ya utekelezaji wa usambazaji wa umeme kwenye maeneo ya vijiji na Kata za  Iparamasa pamoja  Kalembela wakati alipokuwa akizungumza na wananchi kwenye mojo kati ya ziara zake za kukagua utekelezaji wa usambazaji wa umeme wa REA awamu ya tatu.

Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Chato,Dk Medard Kalemani akisalimiana na baadhi ya viongozi pamoja na wananchi wakati alipowasili  kwenye viwanja vya kijiji na kata ya Iparamasa kwaajili ya kuzungumza na wananchi.

Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Chato,Dk Medard Kalemani akiwatunza wanakwaya wa kwaya ya kijiji cha iparamasa.

Meza kuu ikiongozwa na viongozi mbali mbali akiwemo Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Chato,Dk Medard Kalemani.

Diwani wa kata ya Iparamasa Amos Jiji akielezea namna ambavyo wananchi wameendelea kupata changamoto kutokana na kukosa umeme kwa muda mrefu. 

Wananchi wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa waziri wa Nishati ,Dk Medard Kalemani.
Na,Joel Maduka ,Chato

Waziri wa Nishati,Dkt Medard Kalemani amemwagiza mkandarasi shirika la White City  Internationala mbaye anasambaza umeme wa rea awamu ya tatu kwenye Vijini na kata za Iparamasa na Kalembela kuhakikisha anafanya kazi hiyo kwa haraka zaidi ili kuwasaidia wananchi ambao wamekuwa na kilio cha muda mrefu cha uhitaji wa nishati ya umeme.

Hayo aliyasema wakati alipokuwa kwenye ziara ya Kukagua na kuangalia utekelezaji wa mradi wa usambazaji umeme vijijini  Wilayani Chato.

Ambapo Diwani wa kata ya Iparamasa Amos Jiji ,amemweleza Waziri wa nishati ambaye pia ni mbunge wa Jimbo hilo matatizo ambayo yameendelea kujitokeza kutokana na kukosekana  kwa umeme kwenye  kata yake  na kwamba kwa sasa kuna nguzo ambazo zimekaa kwa muda wa miezi mitatu bila ya kusambazwa kwa wananchi ambao wanashida na huduma hiyo.


 Mmoja kati ya wananchi wa kata hiyo ,Bw Peter Mabula ameelezea kukosekana kwa umeme ni chanzo kikubwa ambacho kinakwamisha utendaji kazi hususani kwa upande wa biashara kutokana na wengi wao kutegemea nishati hiyo ili waweze  kuendesha  biashara  zao.


Aidha kutokana na maombi hayo kutoka kwa Diwani pamoja na wananchi Mbunge wa Jimbo la Chato na waziri wa nishati Dk Kalemani alitoa maagizo  kwa Mkandarasi kuhakikisha nguzo ambazo zimelala ndani ya miezi mitatu zisimame na kufikia siku ya alhamisi vijiji hivyo na kata hizo ziwe zimepata umeme.

“Nimesikia kuwa nguzo zimelala tu chini ndani ya miezi mitatu na kwamba mkandarasi alivyosikia nakuja ndio ameanza kazi sasa namwagiza kuwa ahakikishe alhamisi wiki ijayo awe amewasha umeme kwenye kata ya iparamasa na vijiji vyote na mimi siondoki hapa nitahakikisha namsimamia”Alisisitiza Kalemani.

Mradi wa usambazaji wa umeme vijijini  Mkoani Geita,unatekelezwa na mkandarasi  wa Shirika la White City  International ambapo unatarajia kufanyika ndani ya miezi  16 kwenye jumla  vijiji  220 vilivyopo  mkoani humo na jumla ya fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza mradi huo ni  Sh Bilioni 78.56.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa