DHAHABU ZA MIL 700 ZAKAMATWA ZIKISAFIRISHWA KWA MAGENDO.
Jumla ya Gramu 3263.72 za dhahabu zenye thamamani ya
waliokamatwa wakiwa na dhahabu hizo wakisafirisha kwa
njia za magendo pia kinyume cha sheria kwa kutumia gari
aina ya Toyota Premio yenye namba za usajili T.739 EEH mali ya
wilaya ya Ilemela Mwanza, Moshi Manzili (26), Mkazi wa Bariadi
saa 5 usiku katika Mtaa wa Kapera Wilayani Bukombe baada
ya Jeshi la Polisi kupata taarifa za siri na kuweka mtego
uliofanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa hawa. Baada
ya upekuzi wa gari kufanyika, walikutwa wakiwa na kiasi
nyingine unaendelea kufanyika sambamba na kubaini
na kuwakamata watakaobainika kujihusisha na uhalifu huo
moja kujihusisha na vitendo vya magendo na biashara
haramu kwani halitasita kuchukua hatua kali za kisheria
kwa yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo hivyo.
RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKABIDHI TUZO KWA NSSF YA USIMAMIZI NA URATIBU WA HIFADHI YA JAMII KWA SEKTA BINAFSI NCHINI
DC MASALLA ASHAURI MAONESHO YA NANENANE YAVUTIE ENEO LA MAZIWA MAKUU
Rai hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masalla alipotembelea baadhi ya mabanda na kujionea na kupata taarifa mbalimbali kutoka kwa washiriki na kuhimiza fursa ya Mwanza kuwa eneo la kimkakati itumike vizuri kuyapa wigo maonesho hayo.
"Mwanza siku chache zijazo itazidi kuimarika hasa katika eneo la usafiri kuanzia wa anga,reli na barabara hivyo ni wakati mwafaka kwa waandaaji kuja na ubunifu wenye sura ya kimataifa utakao leta tija ya kiuchumi.
Amesema ukanda huu wa nchi za maziwa makuu umejaa wakulima na wafugaji,na makundi mengine na katika maonesho haya kuna utoaji wa elimu ya kitaalamu namna ya kupata tija hata ukiwa na mifugo michache au kuvuna mazao bora kwa muda mfupi bila kitegemea mvua.
Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amewataka Taasisi mbalimbali zinazotoa huduma za Utafiti wa kilimo kwa ujumla ziongeze huduma hizo kwa wakulima wote nchini kutokana na sekta hiyo kuingiza fedha nyingi hivi sasa.
Viongozi mbalimbali wanaendelea kuyatembelea maonesho hayo yatakayo fikia tamati Agosti 8 mwaka huu.
Kauli mbiu ya maonesho hayo ni”chagua viongozi bora wa Serikali za mitaa kwa maendeleo endelevu ya kilimo,mifugo na uvuvi.”
RAS GEITA AYAZINDUA RASMI MAONESHO YA NANENANE KANDA YA ZIWA MAGHARIBI.
Akifungua maonesho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita,Katibu Tawala wa mkoa huo Mohamed Gombati amesema Jukwaa hilo liendelee kuwa somo kwa makundi mbalimbali yanayolengwa na maonesho hayo.
Akiwa na mwenyeji wake Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Bw.Balandya Elikana,Gombati amatembelea mabanda mbalimbali na kujionea huduma zitolewazo na Taasisi,Halmashauri na makundi mbalimbali.
"Serikali ya Rais Samia ni kutaka Taifa lijitosheleze kwa chakula,uwekezaji katika kilimo na maendeleo ya viwanda, nimeona fursa hizo kutokea hapa Nanenane,"amesisitiza Gombati
Akitoa taarifa ya maonesho hayo Bw.Balandya amebainisha yamekuwa na tija kwa wajasiriamali kutokana na kupata elimu ya utaalamu namna ya kuendesha shughuli zao.
"Eneo letu idadi kubwa ni wafugaji na wavuvi,Serikali inaendelea kuwekeza katika sekta hii hivyo wakulima wanafaidika kwa kufanya shughuli zao kwa tija",Balandya.
Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Emil Kasagara amebainisha maonesho ya mwaka huu hadi siku ya jana walikuwa na washiriki zaidi ya 5,000 wakitoa huduma mbalimbali.
Maonesho hayo yatafikia kilele Agosti 8 mwaka huu na mgeni rasmi atakuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda
VICTORIOUS CENTRE CENTER OF EXCELLENCY WAWEKA MIKAKATI KUWASAIDIA WENYE USONJI


WANAFUNZI NAMNA PEKEE YA KUMLIPA RAIS SAMIA NI KUSOMA KWA BIDII-KATIMBA
NAIBU WAZIRI Ofisi ya Rais TAMISEMI (Elimu), Mhe. Zainab Katimba ametoa rai kwa wanafunzi wote nchini kuhakikisha wanasoma kwa bidii na kufaulu kwa viwango vya juu ili badae walitumikie taifa.
Mhe.Katimba ametoa rai hiyo alipotembelea shule mpya maalum ya wasichana ya sayansi ya Mkoa wa Geita kwa lengo la kukagua miundombinu iliyojengwa na kujionea maboresho yaliyofanywa na serikali katika ujifunzaji na ufundishaji kwenye sekta ya elimu nchini.
Amesema kuwa dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha watanzania wanapata elimu iliyobora katika mazingira mazuri hivyo ni wajibu wa wanafunzi kusoma kwa bidii ili kutimiza malengo yao.
“Namna pekee ya kumlipa Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha na kujenga miundombinu iliyobora na kuhakikisha mnapata elimu bila ada ni kuhakikisha na ninyi mnasoma kwa bidii, mfaulu vizuri na kupata elimu bora ili baadaye muweze kulitumikia taifa.”
Katimba amesema wanafunzi wanapaswa kutambua kuwa Taifa linawategemea, hivyo amewataka kuhakikisha hawafanyi mchezo wakiwa shuleni bali watumie fursa hiyo kujenga kesho yao.
Akitoa taarifa ya elimu Mkoa wa Geita, Katibu Tawala Mkoa huo, Mohamed Gombati amesema kwa upande wa shule ya sekondari ya wasichana imepokea Sh bilioni 3 katika awamu ya kwanza na Juni mwaka huu zimepokelewa Sh bilioni 1.1 kwa ajili ya kukamilisha baadhi ya majengo na tayari imeshaanza kuchukua wanafunzi.
Amesema kwa mwaka 2021/22 Mkoa wa Geita ilipokea Sh bilioni 17, mwaka 2022/23 zilipokelewa Sh bilioni 31 na kwa mwaka 2023/24 zilipokelewa Sh bilioni 32 bila kujumuisha fedha zinazotolewa kugharamia elimu bila ada.
Amesema kuwa katika fedha za ndani zinazoelekezwa kwenye miradi ya maendeleo za asilimia 60 au 40 kiwango kikubwa kinaelekezwa kwenye sekta ya elimu.
Awali, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya sayansi ya Mkoa wa Geita, Mwamin Kagoma amesema shule hiyo imegharimu Sh bilioni 4 na mpaka sasa wanafunzi 172 kati ya 211 waliopangiwa kujiunga na kidato cha tano wameripoti shuleni.

%20NSSF.jpg)




.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)







