Home » » RAS GEITA AYAZINDUA RASMI MAONESHO YA NANENANE KANDA YA ZIWA MAGHARIBI.

RAS GEITA AYAZINDUA RASMI MAONESHO YA NANENANE KANDA YA ZIWA MAGHARIBI.

Maonesho ya Nanenane 2024 Kanda ya Ziwa Magharibi yamezinduliwa rasmi leo Agosti 3,2024 kwenye viwanja vya Nyamhongolo huku yakionesha kuzidi kupata hamasa kutoka kwa wananchi.

Akifungua maonesho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita,Katibu Tawala wa mkoa huo Mohamed Gombati amesema Jukwaa hilo liendelee kuwa somo kwa makundi mbalimbali yanayolengwa na maonesho hayo.

Akiwa na mwenyeji wake Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Bw.Balandya Elikana,Gombati amatembelea mabanda mbalimbali na kujionea huduma zitolewazo na Taasisi,Halmashauri na makundi mbalimbali.

"Serikali ya Rais Samia ni kutaka Taifa lijitosheleze kwa chakula,uwekezaji katika kilimo na maendeleo ya viwanda, nimeona fursa hizo kutokea hapa Nanenane,"amesisitiza Gombati

Akitoa taarifa ya maonesho hayo Bw.Balandya amebainisha yamekuwa na tija kwa wajasiriamali kutokana na kupata elimu ya utaalamu namna ya kuendesha shughuli zao.

"Eneo letu idadi kubwa ni wafugaji na wavuvi,Serikali inaendelea kuwekeza katika sekta hii hivyo wakulima wanafaidika kwa kufanya shughuli zao kwa tija",Balandya.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Emil Kasagara amebainisha maonesho ya mwaka huu hadi siku ya jana walikuwa na washiriki zaidi ya 5,000 wakitoa huduma mbalimbali.

Maonesho hayo yatafikia kilele Agosti 8 mwaka huu na mgeni rasmi atakuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda

 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa