Home » » TAKUKURU, WANAFUNZI WAJITOLEA DAMU

TAKUKURU, WANAFUNZI WAJITOLEA DAMU

TAASISI ya kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) wilaya ya Chato mkoani Geita kwa kushirikiana na wanafunzi wa vilabu vya wapinga rushwa  kwenye shule za sekondari wamelazimika kujitolea damu kwa hiari ili kuokoa maisha ya wagonjwa wanaofika katika Hospitali ya wilaya hiyo.

Hatua hiyo inakuja kufuatia Hosptali hiyo kukabiliwa na uhaba mkubwa wa damu salama hali inayotishia maisha ya wagonjwa wenye mahitaji ya huduma hiyo muhimu.

Mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Chato Dk,Pius Buchukundi, amesema kuwa hali hiyo inekuwa ikisababisha ongezeko la vifo vya wagonjwa wenye mahitaji ya huduma hiyo kutokana na jamii kushindwa kuchangia damu kwa hiari ili kuokoa maisha ya wahitaji.

Aidha Kamanda wa Takukuru wilaya ya Chato,David Ringia, amesema taasisi yake baada ya kuguswa na tatizo kubwa la ukosefu wa huduma ya damu salama kwenye hospitali ya wilaya hiyo,na kwa kutambua kuwa inauwezo wa kutoa elimu kwa jamii mbali na kukamata rushwa, waliamua kushirikiana na wanafunzi kusaidia kupatikana kwa huduma hiyo muhimu.

Amesema walishirikiana na wanafunzi wapinga rushwa kutoka shule ya sekondari,Bwina,Wema, Jikomboe na Chato ambapo chupa 17 za damu salama zimepatikana huku akiahidi kuendelea kuielimisha jamii umuhimu wa kutoa damu kwa ajili ya wengine.

Awali mganga mkuu wa hospitali hiyo,amesema zaidi ya chupa za damu salama 400 zinahitajika kila mwezi ili kuwahudumia wagonjwa wanaofika kupata huduma hiyo kila siku badala ya chupa 10 hadi 25 zinazopatikana .

Ametaja baadhi ya magonjwa yanayo changia uhitaji mkubwa wa damu kuwa ni Malaria,Minyoo,utapia mulo pamoja na baadhi ya mama wajawazito wanaofika kujifungua na kutokwa na damu nyingi.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa