Home » » MWENYEKITI MBARONI KWA UCHOMAJI NYUMBA

MWENYEKITI MBARONI KWA UCHOMAJI NYUMBA

JESHI la Polisi wilayani Chato linamshikilia Mwenyekiti wa Kitongoji cha Elimu, Paschal Antony kwa mahojiano kwa tuhuma za kuchoma kaya saba na kuziteketeza kwa moto kwa imani za kishirikina.
Baadhi ya wanakijiji wamekimbia makazi yao baada ya kupata taarifa za uwepo wa jeshi hilo, huku wengine wakirejea kwa kujifichaficha wakihofia kukamatwa.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kakeneno, Kata ya Buziku, James Mlomba, amethibitisha kukamatwa kwa mwenyekiti huyo.
“Inadaiwa Jumapili mwenyekiti huyo alionekana kwenye msiba wa Dagala Ndilo aliyefiwa na mtoto wake na kisha kuonekana kuwa na kikao na baadhii ya watu na baada ya muda wananchi waliandamana kwenda kuchoma nyumba hizo,” alisema Mlomba.
Mtendaji wa kijiji hicho, Emili Mwijarubi, alipoulizwa kuwa alikamatwa pamoja na mwenyekiti huyo na baadae kuachiwa, alikana na kusema yeye ndiye aliyetoa taarifa polisi uwepo wa tukio hilo.
Alisema Jumanne iliyopita Ofisa Upelelezi wa Wilaya ya Chato alifika katika eneo lao na  kumchukua mwenyekiti huyo.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, kaya tano zilichomwa moto na wananchi kwa madai ya ushirikina na kwamba kabla ya tukio hilo kulikuwa na mkutano wa kuwapigia kura watu wanaodhaniwa kuwa ni washirikina.
Kaya tano zilichomwa Jumapili, na siku nyingine zilichomwa nyingine mbili.
 Chanzo;Tanzania Daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa