Leseni hizo zinazokusudiwa kufutwa ni zile zilizotolewa na Serikali kupitia wizara hiyo mwaka 2008.
Kusudia hilo linakuja baada ya Waziri wa Nishati
na Madini, Prof Sospeter Muhongo kutoa notisi ya siku 45 kwa wamiliki wa
leseni hizo kujieleza kwa nini wasifutiwe kutokana na kushindwa kufuata
sheria hiyo.
Akizungumza kwenye mkutano wa Chama cha Wachimbaji
Wadogo wa Madini mkoani Geita (GEREMA)kilichofanyika jana kwenye Hoteli
ya Katoma, Mtaalamu wa Miamba ya Madini, Moses Sagiko kwa niaba ya
Ofisa Madini Mkazi Kanda ya Geita, Juma Sementa, alisema notisi hizo
zimetolewa tangu Januari 14, mwaka huu.
Alisema hatua hiyo ya Waziri Muhongo kutoa hati ya
kuzifuta leseni hizo ni kwa mujibu wa kifungu cha sheria ya madini
namba 13(1) ya mwaka 2010, ambapo leseni ya wachimbaji wadogo
wanaoshindwa kutekeleza taratibu na sheria za leseni hufutwa.
Sagiko alifafanua kuwa sababu kuu mbili kwa
Serikali kukusudia kufuta leseni hizo, moja ni baada ya wamiliki wake
kushindwa kuendeleza shughuli za uchimbaji na uzalishaji katika maeneo
yao kinyume na kifungu cha sheria Na.52 cha sheria ya madini.
Alisema sababu ya pili ni kushindwa kuchukua hatua
mahususi za kulinda na kuendeleza mazingira kinyume cha sheria ya
madini kifungu cha 12c na kushindwa kutoa taarifa za uzalishaji.
Kwa mujibu wa Sagiko alisema mwezi uliopita
serikali kupitia ofisi ya waziri Muhongo ilifuta leseni zaidi ya 100
kutokana na wamiliki wake kukiuka taratibu na sheria za leseni za
uchimbaji wamadini.
Awali mwenyekiti wa chama cha wachimbaji mkoa wa
Geita(GEREMA),Christopher Kadeo alisema wamiliki wa leseni hao
wameshindwa kuziendeleza leseni zao kutokana na kuwa na tamaa ya
kujipatia utajiri wa haraka kwa kuingia mikataba na kampuni za kitapeli.
Kadeo alisema kampuni hizo ziliwarubuni baadhi ya
wamiliki wa leseni hizo kubadili leseni zao kutoka leseni za uchimbaji
mdogo(PML),kuwa leseni za uchimbaji mkubwa(ML) ili kuingia mikataba bila
kujua madhara ambayo yameanza kujitokeza.
Aidha alisema ,GEREMA katika mkutano huo iliwataka
wachimbaji hao walioandikiwa hati wajibu hoja za waziri Muhongo na
kwamba chama cha wachimbaji mkoa kitakuwa nyuma yao kuhakikisha
kinawanusuru wasifutiwe leseni.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment