Home » » ‘Watakaowakopesha wakulima kuuziwa pamba’

‘Watakaowakopesha wakulima kuuziwa pamba’

Wadau wa Bodi ya Pamba mkoani Geita wamekubaliana kuwa kampuni zilizokopesha pembejeo kwa wakulima ndizo zitakazopewa leseni ya kununua pamba kwa kuzingatia ushiriki wa kampuni hizo katika kilimo cha mkataba.
Azimio hilo lilikuja baada ya baadhi ya kampuni kushindwa kukopesha wakulima dawa za kuua wadudu, licha ya kuingia mkataba na Serikali na kukubaliana kampuni hizo kukopeshwa dawa na Bodi ya Pamba, kisha nao wakafanye hivyo kwa wakulima lakini walikiuka maagizo hayo.
Akizungumza jana wakati akifunga kikao cha kawaida cha Bodi ya Pamba, Mweyekiti wa Bodi hiyo ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Said Magalula alisema, dawa za kuua wadudu zilitolewa na bodi ya pamba kwa mkopo kupitia kampuni ya kusambaza pembejeo, ili yakawakopeshe wakulima badala yake walichukua dawa hizo na kwenda kuziuza katika maduka binafsi na wauza maduka hayo kuwauzia wakulima kwa bei ya juu.
Alisema kutokana na hujuma hiyo, bodi iliafikiana kuwauzia pamba kampuni ambazo zitatoa mikopo kwa wakulima na zitakazoshindwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
“Nitoe onyo kwa wanaopeleka viua wadudu hivyo kwenye maduka binafsi waache huo ni wizi na hatutawauzia pamba kampuni ambayo haikumkopesha dawa mkulima,”alisema Magalula.
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa