Na, Magreth Akinyi Ogolla,Geita
yetu blog
MKUU
wa mkoa wa Geita Magalula Said Magalalula amewataka majaji na
mahakimu wa mikoa ya Mwanza na Geita kuendelea kuhukumu kesi za
wananchi wa mikoa hiyo bila kujali masikini au tajiri,na kuacha
kurundika mafaili ya kesi kama ilivyosasa.
Bw
Magalula aliyasema hayo kwenye mkutano wa chama cha majaji[4] pamoja
na mahakimu zaidi ya sabini kinachojulikana kwa jina la Judges
Magistrates Association of Tanzania[JMAT] waliotoka mikoa ya Mwanza na Geita uliyofanyika katika ukumbi wa Alifendo
Hotel mjini hapa.
Amesema
kuwa mahakimu wengi wamekuwa wakiitendea haki taaluma yao kwa kutoa
hukumu za haki ila baadhi yao wamekuwa wakiangalia na kuwapendelea wale
watu wenye unafuu wa maisha kwa kutoa hukumu za upendeleo.
"hii ni taaluma yenu ambayo kwa hakika hampaswi kuingiliwa na mtu katika kutoa maamuzi yenu,niseme walio wengi wanafanya haki kwa kutoa maamuzi ambayo hayana upendeleo,lakini wengine wanaangalia huyu masikini ananyimwa haki yake hii hapana" alisema Magalula
"hii ni taaluma yenu ambayo kwa hakika hampaswi kuingiliwa na mtu katika kutoa maamuzi yenu,niseme walio wengi wanafanya haki kwa kutoa maamuzi ambayo hayana upendeleo,lakini wengine wanaangalia huyu masikini ananyimwa haki yake hii hapana" alisema Magalula
Katika
kikao hicho aliwataka majaji hao kadhalika na mahakimu kutumia mkutano
huo kujifunza na kurekebisha mapungufu na changamoto wanazokabiliana
nazo ikiwa ni pamoja na kuendelea kuharakisha usikilizwaji na kutoa
hukumu za kesi hizo kwa muda muafaka ili
kupunguza mlundikano wa kesi mahakamani na mahabusu huko
magerezani.
"tusaidieni kupunguza huu mrundikano wa mahabusu magerezani kwa kusikiliza kesi zao kwa wakati ,zile kesi ambazo ushahidi umekamilika zifanyie kazi tafadhali" aliongeza Mkuu wa mkoa
Mkutano huo uliokuwa na lengo la kutoa elimu jinsi ya kutatua migogoro ya ndoa pamoja na mirathi.
"tusaidieni kupunguza huu mrundikano wa mahabusu magerezani kwa kusikiliza kesi zao kwa wakati ,zile kesi ambazo ushahidi umekamilika zifanyie kazi tafadhali" aliongeza Mkuu wa mkoa
Mkutano huo uliokuwa na lengo la kutoa elimu jinsi ya kutatua migogoro ya ndoa pamoja na mirathi.
Naye
Aishiel Sumari ambaye ni jaji mfawidhi Mahakama ya kanda ya Mwanza
alimshukuru
mkuu wa mkoa wa Geita kwa kukubali kuwa mgeni rasmi na kuahidi
kuyafanyia kazi yote yaliyosemwa na mkuu huyo na kuidi kuwachukulia
hatua kali mahakimu watakaobainika wanajihusisha na vitendo vya kuomba
na kuchukua rushwa kwenye mahakama mbalimbali za kanda ya Mwanza.
Aidha
Jaji Sumari aliongeza kuwa pamoja na hayo kumekuwa na changamoto
mbalimbali zizowakabili
ikiwa ni pamoja na kukosa ofisi na vitendea kazi kuwa vichache kwenye
mahakama mbalimbali za kanda ya Mwanza na Geita huku akitolea mfano
wilaya ya Nyang'wale iliyopo mkoani Geita ambayo haina ofisi hata moja,
na kumuomba kusaidiwa pale watakapoomba msaada..
0 comments:
Post a Comment