Home » » Hot news: Ocd atuma kikosi kumjeruhi mwandishi,vifaa vyake vya kazi havionekani! vigogo wa polisi wapimpigia magoti mwandishi aliyejeruhiwa kuomba msamaha‏

Hot news: Ocd atuma kikosi kumjeruhi mwandishi,vifaa vyake vya kazi havionekani! vigogo wa polisi wapimpigia magoti mwandishi aliyejeruhiwa kuomba msamaha‏


NA Mwandishi wetu Geita  03.12.2013


MWANDISHI  wa   Habari wa Redio Free Afrika,na magazeti ya Mwananchi na Citizen, Mkoa  Geita  Bwana Salum Maige  amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Geita, baada ya kuumizwa vibaya kutokana na  kushambuliwa  na kundi la askari Polisi wa Kituo cha Polisi Geita wakati akitoka kutekeleza majukumu yake.


Akizungumza  tukio hilo Bwana Maige ambaye amelwazwa katika chumba namba 4 wodi  namda 2 amesema  alishambuliwa juzi majira ya saa moja na dakika 45 usiku, na kundi la  askari polisi zaidi ya wanane karibu na zilipo ofisi za polisi mkoa pamoja na ofisi ya mkuu wa mkoa.


Amedai siku hiyo akiwa  katika maeneo hayo wakati  akielekea nyumbani kwake  mtaa wa Bomani, alikutana na kundi  hilo la polisi walikuwa na gari lenye namba za usajili PT 1998 OCD GEITA, ambapo baadhi yao walishuka kutoka kwenye gari na  kumueleza kwamba yuko chini ya ulinzi  anahitajika polisi.


Amesema  alilazimika  kuwauliza polisi kosa lililosababisha  ahitajike polisi, lakini badala ya kumjibu walimshika na  kumfunga pingu mikononi kisha kumtupia ndani  ya gari na kuanza kumshambulia kwa vipigo.


Maige  amejeruhiwa  vibaya  jicho la upande wa kushoto ambapo kwa  mujibu wa Daktari aliyemfanyia uchunguzi kwenye jicho amesema amepasuka mishipa kwa ndani kutokana na kipigo hali iliyosababisha damu kuvujia ndani ya jicho.


Akifafanua Maige amesema  katika siku za hivi karibuni amekuwa katika mgogoro wa kifamilia na Mkewe, hali iliyosababisha  mkewe kwenda  kumshitaki polisi, ambapo polisi waliamua kwenda  kumkamata  kabla hata ya kumfungulia mashitaka, na baada ya kufikishwa polisi ndipo alipomkuta mkewe na kuanza  kumfungulia mashitaka.


Hata hivyo katika hali ya  kushangaza pamoja na  kujeruhiwa polisi walikataa kumpatia fomu namba tatu (PF3) kwa ajili ya kwenda kupata matibabu hali iliyosababisha kushindwa  kupata matibabu, hadi jana asubuhi ambapo baadhi ya waandishi walilazimika kwenda naye polisi na kudai apatiwe fomu hiyo na kwenda kupatiwa matibabu.


Kamanda wa polisi Mkoa Geita Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Leonard Paulo hakupatikana jana  kuzungumzia tukio hilo la shambulio dhidi ya Mwanahabari huyo, lakini Kaimu wake ACP Pudensiana Protas alithibitisha  kupewa taarifa juu ya kukamatwa kwa mwandishi huyo lakini  hakujulishwa juu ya kushambuliwa kwake.
Hata hivyo baada ya kuoneshwa picha za majeraha ya mwandishi huyo ofisini kwake alionekana kushituka na kuahidi kwenda  hospitalini kufanya mazungumzo na mwandishi huyo, na kwamba  baada ya hapo atafuatilia suala hilo kabla ya kulitolea maelezo ya kina.

Katika tukio hilo Maige anadaiwa kupoteza vifaa vyake vya kazi,kamera aina ya Canon yenye thamani ya Tsh 350,000/=,voice recoder yenye thamani ya Tsh 150,000/=  Hela tasilimu Tsh 16,000/= pamoja na kiambulisho cha kazi .

"mfukoni nilikuwa na kamera,voce recoder na hela elfu kumi na sita
 na wakati wananibeba vilidondoka nikawaambia jamani nimedondosha vitu vyangu, badala ya kunisikiliza nilinaswa kofi na askari mmoja,sijui kama kuna mtu alivichukua au lahh!" alidai Maige

Imeelezwa kuwa muda mfupi kabla ya tukio la kumshambulia Mwandishi huyo,gari lililotumika alikikuwa nalo Mkuu wa polisi wilaya Mrakibu mwandamizi wa polisi Bwire ambaye alikuwa akiendesha mwenyewe maeneo ya mtaa wa Nyerere karibu na "Classic Pub"

Mwandishi wa habari hizi ameshuhudia baadhi ya vigogo wakipishana maeneo ya hospitali ya wilaya akiwemo Mkuu wa upelelezi wa jinai mkoa wa Geita Kamishina wa  polisi Franco Kibona wakifanya jitihada za kumbembeleza Mwandishi aliyejeruhiwa ili yaishe, huku akikiri kuwa vijana wao walifanya kosa kumpiga

" unasikia Maige hawa vijana wetu wamekosea sana maana wewe hakuna hasiyekufahamu,naomba utusamehe kwa hili wewe ni mtani wangu" alidai Mkuu wa upelelezi mkoa.


Habari na Geita yetu Blog

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa