Home » » SHULE YENYE ZAIDI YA WANAFUNZI 500 HAINA VYOO GEITA WANAFUNZI

SHULE YENYE ZAIDI YA WANAFUNZI 500 HAINA VYOO GEITA WANAFUNZI

 zaidi ya wanafunzi 500 wanaosoma shule ya msingi Nyang’homango katika kata ya Ilemela wilayani Chato mkoani Geita hawana mahala pa kujisaidia baada ya vyoo walivyokuwa wakitumia kutitia na kubomoka kutokana na kujengwa chini ya kiwango.
 Hali hiyo imeelezwa kwenye mkutano mkuu wa dhalula wa kijiji na mwalimu mkuu wa shule hiyo Bw. Gilbert Edward ambaye amesema hali hiyo inahatarisha maisha ya wanafunzi hao. Amesema vyoo hivyo vilijengwa mwaka 2002 na serikali kupitia mpango wa HESAWA lakini havikuwa na ubora kutokana na kujengwa bila kuwekewa nondo hali ambayo imesababisha vititie. 
 Kwa upande wake diwani wa kata ya Ilemela wilaya Chato Bw. Ismail Luge amewataka wananchi hao kuchukua hatua za haraka kujenga vyoo vingine hali itakayosaidia wanafunzi hao kujisaidia watakapokuwa wamefungua shule.
 Ili kuunga juhudi hizo za ujenzi wa vyoo vipya diwani Luge amechangia mifuko mitano ya saruji huku wanakijiji wakitakiwa kuchangia shilingi 13,000 kwa kila mwenye uwezo wa kufanyakazi kwa lengo la kukamilisha shilingi milioni tatu kwa ajili ya ujenzi huo.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa