Home » » KANGI LUGOLA ASWEKA NDANI VIGOGO WATANO WA MGODI AKIWEMO MZUNGU KWA UKIUKAJI WA SHERIA YA MAZINGIRA

KANGI LUGOLA ASWEKA NDANI VIGOGO WATANO WA MGODI AKIWEMO MZUNGU KWA UKIUKAJI WA SHERIA YA MAZINGIRA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais Inayoshughulika na muungano na Mazingira Mheshimiwa Kangi Lugola akizungumza na wananchi ambao mashamba yao yameathirika kutoka na sumu ambayo imeeharibu mazao yao pamoja na viumbe hai.
Moja kati ya wakurugenzi wa Mgodi wa  Nyarugusu Mine Co.Limited  Fred Masanja akionesha cheti NEMC ambacho naibu waziri alikikata.

Bwawa la kuhifadhia maji ya kemikali ambalo limeharibika na kusababisha maji mengi kuelekea kwenye shughuli za wananchi.

Naibu Waziri wa Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais Inayoshughulika na muungano na Mazingira Mheshimiwa Kangi Lugola ,akiwa na mwenyeji wake ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Geita wakikagua eneo ambalo lilipasuka na kupeleka maji ya sumu kwenye maeneo ya mashamba ya wananchi.

Naibu Waziri wa Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais Inayoshughulika na muungano na Mazingira Mheshimiwa Kangi Lugola  akiangalia baadhi eneo ambalo limepasuka.

Naibu Waziri wa Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais Inayoshughulika na muungano na Mazingira Mheshimiwa Kangi Lugola  ,akitembelea na kuangalia miche ya miti ambayo imekwisha kuathirika.

]Naibu Waziri wa Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais Inayoshughulika na muungano na Mazingira Mheshimiwa Kangi Lugola ,akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi na baadhi ya wananchi ambao wameathirika kutokana na maji Hayo kwenye maeneo ya mashamba.

(PICHA NA JOEL MADUKA)

Ekari 270 za mashamba ya wakulima kwenye kijiji cha Ziwani Kata ya Nyarugusu Wilayani Geita zimeathiriwa na Sumu iliyotoka kwenye Bwawa la kuhifadhia Kemikali lililopasuka kingo zake na maji kusambaa kwenye mashamba hayo.

Hali hiyo imemlazimu Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Bw Kangi Lugola kuitaka kampuni ya Madini ya Nyarugusu inayohusika na suala hilo kuwalipa fidia wananchi 57 ambao mazao yao yameathirika.

Awali Bw Lugola aliagiza muwekezaji huyo akamatwe kutokana na kile alichodai kuwa ni uvunjifu wa sheria za utunzaji wa mazingira mgodini hapo na kwamba uongozi wa mgodi huo ulimzuia Afisa Mazingira wa Wilaya ya Geita Bi Hellen Eustace kutekeleza majukumu yake baada ya kufika mgodini hapo kukagua namna wanavyozingatia utunzaji mazingira

Bw Kangi alisema Mwekezaji haruhusiwi kuendelea na shughuli anazozifanya na kufunga mgodi huo hadi watakapotekeleza mambo waliyoelekezwa

Mkurugenzi wa Nyarugusu Mine Company Bw Fred Masanja amesema kusimamishwa kwa shughuli zao kunaweza kuathiri ytendaji wao kwa kuwa Tani Laki moja na 20 hawataweza kuzizalisha na hivyo watapata hasara ya zaidi ya Sh Milioni 600 hadi 700

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa