Home » » BENKI YA NMB YAIPA MKONO JAMII YA GEITA

BENKI YA NMB YAIPA MKONO JAMII YA GEITA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa - Abraham Augustino (kulia) akikabidhi madawati kwa Mkuu wa Wilaya ya Geita - Manzie Mangochie (kushoto) kwa niaba ya Shule za Msingi Nyamkumbu na Ukombozi msaada wa madawati 100 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kutoka Benki ya NMB katika hafla fupi iliyofanyika mjini Geita jana ambapo kila shule imekabidhiwa madawati 50.
Wanafunzi wa Shule za Msingi Nyankumbu wakiwa na nyuso za furaha baada ya kukabidhiwa msaada wa madawati 50 na Benki ya NMB jana wilayani Geita. NMB ilisaidia madawati 100 yenye thamani ya Shilingi milioni 10 katika shule mbili za msingi za Nyamkumbu na Ukombozi ambapo kila shule ilipata madawati 50.
Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa - Abraham Augustino (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Geita, Manzie Mangochie (kushoto) pamoja na wanafunzi baada ya makabidhiano ya madawati.

Benki ya NMB jana ilikabidhi msaada wa madawati 100 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa Shule za Msingi Nyankumbu na Ukombozi zilizopo mkoani Geita ambapo kila shule imekabidhiwa madawati 50.

Msaada huo umekabidhiwa na meneja wa NMB Kanda ya Ziwa - Abraham Augustino ambapo mkuu wa wilaya ya geita alipokea madawati hayo kwa niaba ya shule hizo mbili za msingi.

“Madawati haya tunayoyakabidhi leo ni moja ya ushiriki wetu katika maendeleo ya jamii na sisi kama benki inayoongoza Tanzania tunahakikisha jamii inayotuzunguka inafaidika kutokana na faida tunayoipata,” alisema Augustino.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa