Home » » KIGOGO CCM LAWAMANI GEITA

KIGOGO CCM LAWAMANI GEITA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph MsukumaMWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita, Joseph Msukuma, amelaumiwa akidaiwa kuingilia maamuzi yanayofikiwa na Baraza la Madiwani, likiwemo la ujenzi wa choo.
Kutokana na shutuma hizo, baadhi ya madiwani walitishia kuandika barua ya kumtaka waziri mwenye dhamana na mamlaka za miji kuifuta Halmashauri ya Mji wa Geita kwa kile walichodai ‘kuporwa’ uhalali wake wa kujiamria mambo yake kwa mujibu wa katiba.
Diwani wa Bulela, Boniphas Fulano, alimshutumu mwenyekiti huyo kwa madai kuwa amekuwa akiingilia na kuvuruga maamuzi yao. Alidai baraza hilo liliamua kuvunja soko la Shilabela na Nyankumbu yaliyopo barabarani kwa ajili ya usalama wa wananchi, lakini mwenyekiti huyo alienda kuzuia agizo hilo.
Katika mgogoro wa ujenzi wa choo cha wafanyabiashara, kiongozi huyo wa CCM aliamuru kisijengwe kiasi cha kusababisha vurugu.
“Na suala la ujenzi wa choo hiki cha soko kuu baraza lilikaa Aprili 30, mwaka huu na kuamua ufanyike, na akiwa na taarifa za hatua zote, lakini amekuwa akiwaingilia bila kufuata utaratibu wa kiuongozi, hivyo kuonekana halmashauri hii haina maana kuwepo,” alisema Filano.
Hata hivyo, Msukuma alijitetea akidai kuwa alichukua uamuzi huo baada ya kupata malalamiko kwa wananchi kuwa hawajashirikishwa katika ujenzi huo, hivyo alifikia uamuzi wa kufukia mashimo ya msingi yaliyokuwa yameanza kuchimbwa na mkandarasi aliyekuwa amepewa kazi hiyo.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa