Home » » HATARI: Walimu 97 watumia choo kimoja; wanafunzi 3,563 watumia matundu 14‏

HATARI: Walimu 97 watumia choo kimoja; wanafunzi 3,563 watumia matundu 14‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

WALIMU 97 katika shule ya msingi Nyankumbu na Mkombozi katika Wilaya ya Geita, wanatumia tundu moja la choo ambacho kipo kwenye nyumba ya mwalimu huku wanafunzi wa shule hizo 3,563 wakitumia matundu 14 ya choo na kuhofiwa kutokea magonjwa ya milipuko.Taarifa za awali kuhusu tatizo hilo zinadai kuwa, baadhi ya walimu wamekuwa wakiulalamikia uongozi wa halmashauri hiyo kwa muda wa miaka mitano hadi sasa, bila kusikilizwa licha ya uongozi wa shule kuandika barua kwa Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kutaka tatizo hilo kutatuliwa.

Baadhi ya wanafunzi wakiongea na mtandao huu Juni 6, 2014 wamedai kuwa wamekuwa wakipata usumbufu wakati wa kujisomea kutokana na shule hizo kukosa madawati yakutosha na wakati mwingine kuhofia kula vyakula mbalimbali kutokana na hofu ya kupata magonjwa ya milipuko.

Akizungumzia tatizo hilo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi, Nyankumbu, Jasmin Ngume, amesema awali ilikuwa shule moja na baada ya muda uongozi wa Halmashauri hiyo, ilifanya utaratibu wa kuzigawanya na kuwepo na shule ya msingi Mkombozi na Nyankumbu, ambazo hadi sasa zinakabiliwa na matatizo ya miundombinu ya madarasa na vyoo.

“Tangu walivyofanya utaratibu wao tumeendelea kutumia tundu moja kwa walimu wote lakini wanafunzi waligawana matundu Saba kwa kila shule” alisema Ngume.




Shule zetu



Amesema kwa mujibu wa taratibu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, uwiano wa vyoo kanuni zinaeleza kuwa walimu wa kiume wanne wanatakiwa kutumia tundu moja na walimu wa kike watatu wanatakiwa kutumia tundu moja, na wanafunzi wakiume watatu hutumia tundu moja na wakike wanne hutumia tundu moja jambo ambalo halipo katika shule hiyo.



“Hili tatizo limekuwa kubwa kwa maana wakati mwingine wanafunzi wamekuwa wakienda kujisaidia kwenye nyumba za majirani na wakati mwingine wanazuiliwa, jambo ambalo linatulazimu wakati mwingine kuwarudisha nyumbani mapema ili wakajisaidie huku muda wa kazi ukiwa bado ukiwa haujafika”



Licha ya mkoa huo kujitahidi kuboresha miundombinu ya shule zilizopo mkoani humo na usimamizi makini, katika uandikishaji wa wanafunzi wa awali kwa mwaka 2014 asilimia 79.4 ya wanafunzi waliandikishwa, na kwa upande wa darasa la Saba ni asilimia 91 wakati mwenendo wa kuripoti shuleni kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza ni asilimia asilimia 84

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa