Home » » WAZAZI GEITA MBARONI KWA KUTOPELEKA WATOTO SHULE

WAZAZI GEITA MBARONI KWA KUTOPELEKA WATOTO SHULE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAZAZI watano mkoani Geita wamekamatwa na Polisi kwa kugoma kuwapeleka watoto wao shule na kuwalazimisha kuwaoza.
Hatua hiyo inatokana na agizo la Mkuu wa Mkoa wa Geita, Saisi Magalula, la kuwataka watendaji kuwakamata wazazi na walezi wasiopeleka watoto wao shule.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mtendaji wa Kata ya Ihanamilo, Aaron Ngoye, alisema amewakamata na kuwapeleka wazazi hao polisi kutokana na kukaidi agizo hilo.
Aliwataja wazazi waliokamatwa  kuwa ni Daud Hassan, Ezila Razaro,  Ramadhani Juma, Mbotolo Kabanzi na Hakiyamungu Kabinza, wote wakazi wa Kata ya Ihanamilo na kwamba watafikishwa mahakamani wakati wowote kujibu shitaka hilo.
Alisema ingawa kuna changamoto nyingi kama kukosana na wazazi na walezi wakidai watoto si wa mtendaji, lakini amekuwa akiwakamata wazazi hao.
Hata hivyo, alisema kwa sasa baadhi ya wazazi wana uelewa kidogo wa kuwasomesha watoto wao.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa