Home » » ALALAMIKIA GGM KUMPORA ARDHI

ALALAMIKIA GGM KUMPORA ARDHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KAMPUNI ya Geita Gold Mine (GGM) inatuhumiwa kumpora mzawa, Hosea Katampa, eneo lake lililopo Lijeti namba tatu licha ya kwenda mahakamani kulidai na kupewa kihalali.
Katampa alitoa malalamiko hayo juzi alipozungumza na waandishi wa habari waliofika eneo hilo na kumuomba Waziri wa Nishati na Madini, kuingilia kati  mgogoro huo ili arudushiwe eneo lake.
Alisema mgodi huo ulianza kulichimba eneo lake aliloanza kulimiliki mwaka 1988 bila kuwapo kwa makubaliano yoyote.
Ofisa Mahusiano  wa mgodi wa GGM, Joseph Mangilima, alipoulizwa alisema: “Namfahamu Katampa na kesi yake naijua alishinda  kihalali mahakamani sasa suala la kwa nini hajarudishiwa eneo lake mimi nashindwa kuelewa”.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa