Home » » SERIKALI YAANZA KUTOA LESENI KWA WACHIMBAJI WADOGO GEITA

SERIKALI YAANZA KUTOA LESENI KWA WACHIMBAJI WADOGO GEITA


Geita
HATIMAYE serikali imekamilisha zoezi la upimaji wa viwanja 18 kwenye eneo lenye ukubwa wa Hekta 373.6 katika vijiji vya Isamilo na Nyamikoma wilayani Geita lililotengwa na wizara ya nishati na madini kwa ajili ya wachimbaji wadogo.
Hatua hiyo ni kutokana malalamiko ya muda mrefu ya wachimbaji wadogo kukosa maeneo mazuri ya kuchimba kufuatia baadhi ya wenye leseni kuuza leseni zao kwa wakezaji wakubwa na hivyo kujikuta hawana maeneo mazuri ya kuchimba.
Mkuu wa mkoa wa Geita Said Magalula amesema hayo jana(Jumatatu) alipokutana na waandishi wa habari ofisi kwake ili kuzungumzia sekta hiyo ya madini inayotegemewa na idadi kubwa ya wakazi wa wilaya ya Geita.
Amesema zoezi la upimaji wa viwanja hivyo vilivyochukua ukubwa wa Hekta 83.45 kati ya hekta 373.6 limefanyika baada ya kufanyiwa uchunguzi na watalaamu mbalimbali wa miamba kupitia wakala wa JiolojiaTanzania(GST) na kubaini kuwa eneo hilo lina miamba yenye madini ya dhahabu.
Kufuatia kukamilika kwa zoezi hilo mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wananchi wa Geita kutumia fursa hiyo kutuma maombi ya leseni kwa ofisa madini mkazi kupitia vikundi vyao vya ushirika(SACCOS) na Vijiji na kwamba hakuna leseni itakayotolewa kwa mchimbaji mmjo mmoja.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa