na John Sanjo, Geita
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kanda
 ya Ziwa Magharibi, Peter Makele, amemtaka Diwani wa Kasamwa, Fabian 
Mahenge, kutolipa kisasi kwa waliomsababishia kufungwa akitetea masilahi
 ya Wana Kasamwa.
Kauli ya mwenyekiti huyo ilikuja jana baada ya Mahenge kumaliza adhabu
 ya kifungo cha miezi mitatu kabla ya rufaa yake kukubaliwa, ambapo 
diwani huyo na wenzake watano walifungwa.
Pamoja na diwani huyo, wengine waliotumikia kifungo hicho kwa makosa 
ya uchochezi na kusababisha nyumba ya mganga wa kienyeji kuchomwa moto 
ni Yombo Petro, Zenze Richard, Nomelo Ndikusataga, Nicholaus Buseng'hwa 
na Ngiyu Lung’wecha.
Ilidaiwa kwamba mganga huyo alikaidi agizo la kupisha ujenzi wa kituo cha mabasi mjini Geita.
  Kwa upande wake Mahenge alisema hatarudi nyuma katika kupigania 
masilahi ya wakazi wa kata hiyo huku akisisitiza kwamba atafanya hivyo 
kwa mujibu wa sheria bila woga.
CHANZO: DAIMA 
0 comments:
Post a Comment