Home » » RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA PROF. IBRAHIM GAMBARI MJUMBE MAALUM WA RAIS WA NIGERIA, CHATO MKOANI GEITA.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA PROF. IBRAHIM GAMBARI MJUMBE MAALUM WA RAIS WA NIGERIA, CHATO MKOANI GEITA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
PICHA NA IKULU


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 10 Januari, 2017 amekutana na kufanya mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Rais wa Nigeria Profesa Ibrahim Gambari nyumbani kwake Chato Mkoani Geita. Mazungumzo yao yalilenga masuala mbalimbali ya uhusiano kati ya Tanzania na Nigeria.
Rais Magufuli amempongeza Rais Muhammadu Buhari kwa jitihada kubwa anazochukua kwa ajili ya kuleta maendeleo nchini mwaka.
Pia, Rais Magufuli amempongeza Rais Buhari kwa jitihada anazozifanya za kukabiliana na kundi la Boko haramu ili kuhakikisha amani inaendelea kudumu nchini mwake.
Kwa upande wake Mjumbe Maalum wa Rais wa Nigeria, Profesa Ibrahim Gambari amempongeza Rais Magufuli kwa ushindi alioupata na jitihada anazochukua katika kupambana na rushwa na kubana matumizi jambo ambalo linaungwa mkono na wananchi wengi wa Nigeria.
Profesa Gambari alimkabidhi Rais Magufuli barua yenye ujumbe maalum kutoka kwa Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria.


Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Chato, Geita
10 Januari, 2017

 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa