Home » » WATU 7 WALIOFARIKI KATIKA AJALI YA GARI GEITA SIKU YA MKESHA WA KRISMASI WAZIKWA

WATU 7 WALIOFARIKI KATIKA AJALI YA GARI GEITA SIKU YA MKESHA WA KRISMASI WAZIKWA

Mkuu wa wilaya ya Kahama bw. Fadhili nkulu amewaongoza mamia ya wakazi wa wilaya ya Kahama na viunga vyake katika mazishi ya watu saba waliofariki katika ajali ya gari tarehe 24 mwezi huu katika eneo la Kanegere wilayani Mbogwe mkoani Geita akiwemo Padri wa kanisa katoliki la Mt.Karoli Lwanga mjini Kahama muda mfupi kabla ya mkesha wa sikukuu ya Krismasi kuanza.

Akizungumza katika ibada hiyo iliyoongozwa na askofu Flavian Kasala wa jimbo kuu Katoliki Geita na hudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, dini, siasa na waumini wa madhehebu tofauti ya dini mkuu wa wilaya ya Kahama Bw.Fadhili Nkulu amesema msiba huo umeacha pengo kubwa kwa wana Kahama kwani wamempoteza kiongozi shupavu wa kiroho na vijana ambao walikuwa ni tegemeo licha ya kuwa bado walikua wanafunzi huku akiwataka wasihusishe na imani tofauti zisizostahili.

Naye askofu Liberatus Sangu wa kanisa Katoliki jimbo la Shinyanga amewaasa waumini wa dini zoye kukumbuka kutubu na kuishi maisha ya kumuamini mwenyezi mungu huku Askofu Lidorvic minde wa kanisa Katoliki Parokia ya Mt. Karoli Lwanga Kahama ambako ndiko mazishi yalikofanyika akitoa neno la faraja kwa waombolezaji.

Nao baadhi ya waombolezaji na wau waliohudhuria katika mazishi hayo wameonyesha masikitiko yao na kuzungumzia msiba huo ambao umeonyesha kuwagusa kwa namna moja au nyingine
CHANZO MICHUZI MEDIA GROUP

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa