Home » » TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA MKOA WA GEITA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA MKOA WA GEITA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mhe. Amani K. Mwenegoha amewataka waandishi wa habari nchini kufanya kazi zao kwa ueledi na kwa kuzingatia misingi na maadili ya taaluma za uandishi wa habari wakati wakifanya kazi za uandishi.
Mhe. Amani K. Mwenegoha ameyasema hayo jana akitolea ufafanuzi taarifa zilizoandikwa za upotoshaji zilizotolewa na gazeti la Mwanahalisi iliyoandikwa na mwandishi Ansbert Ngurumo toleo na: 341 la Mei 30 mwaka 2016 siku ya Jumatatu ukurasa wa 10 na 11. yenye kichwa cha habari Ngono na Mwanafunzi yaleta msukosuko Ushirombo mimi kama Mkuu wa Wilaya ya Bukombe nimetuhumiwa kutumia madaraka yangu vibaya kwa kumlinda na kumkingia kifua Afisa Tarafa wa Siloka Bw. Tumbo John Madaraka.
Sikuwahi  Kupokea  barua  yeyote kutoka kwa Matayo Paschal wala kuamrisha akamatwe ,pia sikuwahi  kuzungumza  na  mwandishi  yeyote kuhusu mtoto huyo,wala sijapokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Polisi Bukombe kuhusu mtoto huyo wala malalamiko yoyote kutoka kwa wazazi,mlezi au Mwalimu Mkuu wa Shule  aliyosoma mwanafunzi huyo” alisema Mhe. Mwenegoha
Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Bukombe “amekemea na kulaani kitendo cha mwandishi wa gazeti la Mwanahalisi kuandika habari bila kuzingatia  maadili ya kiuandishi kwa kufika eneo la tukio na kuonana na walengwa sio kuandika habari za kupelekewa au kusikia mtaani, angezingatia  kupata  taarifa kwa pande zote mbili ili kupata taarifa zenye ukweli,uwazi na uhakika”.
Pia ametoa wito kwa waandishi wa habari nchini kuwa wazalendo na kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika  ujenzi wa nchi yetu kwa kufichua uovu utakaorudisha nyuma maendeleo ya jamii yetu  badala ya kuweka vibonzo visivyowakilisha maslahi ya nchi yetu na kuvunja moyo juhudi zinazofanywa na Rais wetu za kuinua Uchumi.
Wakati huo huo, Mkuu wa wilaya ya Bukombe Mhe. Amani K. Mwenegoha amesisitiza wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kutoa taarifa kwa vyombo vya serikali haraka kadri inavyowezekana inapotokea wana tatizo linalouhusiana na watoto wao wanapokutana na changamoto ambazo serikali inaweza kushughulikia na imekua ikifanyika hvyo pale ambapo mzazi,mlezi au jamii inapotoa malalamiko au taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ambapo yamekua yakishughulikiwa na sheria imekua ikichukua mkondo wake.

Imetolewa na
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Bukombe
Geita
03 Juni, 2016
 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa