Home » » CHADEMA KUJIPIMA SERIKALI ZA MITAA

CHADEMA KUJIPIMA SERIKALI ZA MITAA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Bukombe. Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha) limesema uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji utakaofanyika Desemba 14, mwaka huu, utatoa picha halisi ya uwezo wao wa kushika dola katika Uchaguzi Mkuu 2015.
Pia, Chadema imewaomba wananchi wote waliofikisha umri wa kupiga kura kujitokeza kujiandikisha katika daftari la makazi na daftari la kudumu la wapigakura wakati uandikishaji utakapoanza.
Halima Mdee, ambaye ni mwenyekiti wa Bawacha na mbunge wa Kawe, alisema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Kilimahewa wilayani Bukombe mkoani hapa.
Mdee alisema chama hicho kimejiandaa kuchukua dola mwakani, lakini hilo litafanikiwa ikiwa uchaguzi wa serikali za mitaa utatoa dira kamili ya ukombozi wa pili wa taifa.
“Watanzania, uchaguzi huu wa Desemba 14 ndiyo utatoa dira kamili… utakuwa ni uchaguzi muhimu kuliko hata huo wa mwakani wa madiwani, wabunge na urais kwani unapotaka kujenga nyumba madhubuti lazima uanzie msingi imara na ndiyo maana tunasema uchaguzi huu ni muhimu,” alisema.
“Wanawake wenzangu, acheni kuhongwa chumvi na kanga na CCM. Kama wameshindwa kuwaletea maendeleo kwa miaka 52 ya uhuru, ni maendeleo gani tena wanayotaka kuyaleta?” alihoji Mdee huku wananchi wakimjibu, “hakuna, hakuna… wameshindwa”.
Naye katibu mkuu wa baraza hilo, Grace Tendega alisema ifikapo Novemba 23, mwaka huu wananchi wajitokeze kujiandikisha katika daftari la makazi ili kuwawezesha kushiriki ipasavyo katika uchaguzi huo wa vijiji, vitongoji na mitaa.
“Tunawaomba wananchi ambao mmefikisha miaka 18 kujitokeza kwa wingi ili kuanza kuifuta CCM kuanzia ngazi ya chini kwa kuanzia huko ili mwakani wakati wa uchaguzi ujao, tuwe tumewaonyesha mlango wa kuondokea,” alisema Tendega.
Uchaguzi wa serikali za mitaa utafanyika Desemba 14, wakati Uchaguzi Mkuu utakuwa Oktoba mwakani.
kupigiwa kelele na CCM lakini hazina nguvu kutokana na kutodaiwa mahakamani kama hazitatolewa.
“Leo hii eti wanasema kuna haki za watoto, wazee, afya, wasanii lakini wanashindwa kusema kwamba haki hizo Ibala ya 20 (1)(2) zimefungwa kudaiwa makahakani…ikataeni pindi itakapokuja kupigiwa kura ya maoni kwani haina kitu na badala yake maoni yenu yametupwa kando,” alisema Mwaifunga
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa