Home » » WANAWAKE GEITA WATAKA KATIBA IJAYO WAJALI

WANAWAKE GEITA WATAKA KATIBA IJAYO WAJALI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAKATI taifa likiwa kwenye sintofahamu juu ya mchakato wa katiba mpya, wanawake wilayani Geita mkoani hapa wameitaka katiba ijayo kuweka sheria za kujali wanawake, wajane na walemavu.
Wito huo ulitolewa jana na washiriki kwenye mdahalo uliofanyika katika ukumbi wa Kanisa la Katoliki ambao uliandaliwa Geita Network Platfom, ambapo walisema katiba iweke mambo ya kuwajali na kuwalinda wanawake.
Washiriki hao walisema masuala ya wanawake yanapotambulika kikatiba ni rahisi kutungiwa sheria na hivyo matatizo yoyote yanayowakabili hutatuliwa kisheria badala ya kufanyiwa hisani.
Walibainisha kuwa miongoni mwa mambo yanayowakabili ni matukio ya unyanyasaji na udhalilishaji, ikiwemo kubakwa huku kesi zao zikichukua muda mrefu na hivyo ushahidi kupotea.
Joyce Juma, alisema kuwa kumekuwa na vitendo viovu ambavyo wanafanyiwa wanawake bila serikali kuchukua hatua, kwa hiyo akaomba kwenye katiba ijayo yawepo mambo ya kuwalinda na kuwatetea wanawake kwa nguvu zote.
Katibu wa asasi hiyo, Isaka Kubini, alisema wataendelea kuandaa makongamano kama hayo kila wakati ili wananchi waweze kuelewa na kuipigia kura katiba inayopendekezwa baada ya kupitishwa bungeni.
“Tutazidi kuweka makongamano kama haya ili wananchi wawe na uelewa wa wanachokipigia kura ya kukubali au kukataa katiba inayopendekezwa wakati wa upigaji wa kura za maoni,” alisema.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa