Home » » CHADEMA YATETEA WACHIMBAJI WADOGO

CHADEMA YATETEA WACHIMBAJI WADOGO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Geita, wameitaka serikali mkoani hapa kuwatafutia maeneo ya kuchimba wachimbaji wadogo wadogo kuliko kuwaacha wakihangaika na kukumbatia wachimbaji wakubwa pekee.
Mwenyekiti wa  CHADEMA mkoani hapa, Aliphonce  Mawazo, alitoa kauli hiyo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Soko Kuu, huku akiwatuhumu viongozi wa mkoa kwa kushirikiana na Idara ya Madini kutowathamini wachimbaji wadogo wadogo, jambo ambalo amesema ni hatari kwa vijana ambao hawana ajira.
Alisema ingawa wachimbaji wadogo wadogo walipewa maeneo ya kuchimba sehemu ya lwenge, lakini maeneo hayo  hayana dhahabu na wamekuwa wakiilalamikia serikali, ili iwatafutie maeneo ambayo wataweza kupata chochote kwa ajili ya kuendesha maisha yao.
Katibu wa chama hicho, Soud Ntanyanga, alilaani vitendo vinavyofanywa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita kwa kuwaingilia watendaji katika kutekeleza majukumu yao kwa kisingizio cha kwamba chama tawala lazima kitoe maelekezo katika kutekeleza majukumu yake
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa