Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WANAOJICHUKULIA sheria mkononi kwa kuwaua wahalifu na vikongwe kwa
imani za kishirikina mkoani hapa, wametakiwa kuacha tabia hiyo kwa
sababu wanaenda kinyume na neno la Mungu.
Kauli hiyo imetolewa jana na Askofu Mkuu wa Kanisa la Tanzania
Assemble of God (TAG) Jimbo la Geita, Simon Masunga, kwenye mkutano wa
siku nane unaoendelea katika Viwanja vya Kalangalala vilivyoko mjini
hapa.
Askofu Masunga alisema baadhi ya wakazi wa Geita huwa wanajichukulia
sheria mkononi kwa kuwaua vikongwe na wahalifu kwa kuwachoma moto
kutokana na kutomjua Mungu.
Alisema wakazi hao wamejikita kwenye mambo mengi ya kidunia kuliko
kumuweka Mungu mbele, lakini alisema yeye na waumini wanajitahidi
kuwaombea wenye tabia hiyo waokolewe na kuacha dhambi hiyo.
Pia Askofu Masunga aliwakemea wachungaji wanaofungua makanisa kwa
ajili ya uchochezi au kukashifu dini nyingine kwa kuwaambia waache
tabia hiyo na badala yake wafanye kazi ya Mungu.
Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment