Home » » Wanafunzi walalamika kutumia majina bandia

Wanafunzi walalamika kutumia majina bandia

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari Nyugwa, Wilaya ya Nyangh’wale, mkoani Geita, wameiomba serikali ya mkoa kumchukulia hatua Ofisa Elimu ya Sekondari wa wilaya hiyo na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Lucas Joshua, kwa kuuza majina yao kwa watu wakati wakifanya mtihani wa kidato cha pili.
Wanafunzi hao wanadai viongozi hao wamewalazimisha kuwapa majina ya bandia ili kuhalalisha uovu wanaoufanya.
Wakizungumza kwa wakati tofauti juzi, wanafunzi hao walisema Mwalimu Joshua  amekuwa kinara wa kuuza majina yao na kuwapa majina bandia na kuwataka kama wanataka ya kwao yaliyopotea  kuyanunua ni kati ya sh 25,000 hadi 30,000, huku wakiambiwa majina yao ya awali yanafuatwa mkoani kwa pesa.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa