MWANAMKE aliyefahamika kwa
jina la Sambila Mihayo anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 20 hadi
22 ameuawa kinyama na wananchi wenye hasira kali baada ya kukamatwa
akiiba mahindi mabichi shambani katika Kitongoji cha Ilolanguli kijiji cha
Mbabani Wilaya ya Geita mkoani hapa.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo majira ya saa 9:00 usiku ikiwa ni siku moja tu ya watu wote duniani kusherehekea sikukuu ya mwaka mpya wa 2014.
Mwenyekiti wa kitongoji hicho,Abel Kidesheni alifika eneo la tukio hilo na kukuta tayari mwanamke huyo akiwa ameuawa na wananchi hao huku mwili wake wakitaka kuuteketeza kwa moto.
Kidesheni amesema mwanamke huyo alikutwa akikata mahindi kisha kuyapakia kwenye mfuko wa sandarusi ndipo alipokamamatwa na wananchi ambao walimshambulia kwa mawe marungu na fimbo hadi kupoteza maisha yake.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo majira ya saa 9:00 usiku ikiwa ni siku moja tu ya watu wote duniani kusherehekea sikukuu ya mwaka mpya wa 2014.
Mwenyekiti wa kitongoji hicho,Abel Kidesheni alifika eneo la tukio hilo na kukuta tayari mwanamke huyo akiwa ameuawa na wananchi hao huku mwili wake wakitaka kuuteketeza kwa moto.
Kidesheni amesema mwanamke huyo alikutwa akikata mahindi kisha kuyapakia kwenye mfuko wa sandarusi ndipo alipokamamatwa na wananchi ambao walimshambulia kwa mawe marungu na fimbo hadi kupoteza maisha yake.
Kamanda wa Polisi mkoani
Geita,Leonard Paulo amethitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kwamba
uchunguzi unaoendela ikiwa ni pamoja na kuwabaini wote waliohusika na tukio
hilo na kwamba hakuna mtu aliyeshikiliwa kuhusiana na tukio hilo.
Tukio hilo ni pili kutokea
mkoani Geita katika kipindi kisichozidi wiki moja baada ya wanaume watano
kuuawa kwa kukatwa kwa mapanga kisha miili yao kutoeketezwa kwa moto baada ya
kuiba rambi rambi msibani kitongoji cha Nyantorotoro A,mjini Geita.
0 comments:
Post a Comment