Home » » KATIBU WA CCM MKOA WA GEITA AWATAKA VIONGOZI KUWATEMBELEA WANACHAMA‏

KATIBU WA CCM MKOA WA GEITA AWATAKA VIONGOZI KUWATEMBELEA WANACHAMA‏



Na Denice Stephano,Geita yetu Blog

KATIBU wa CCM mkoa wa Geita Mary Maziku amewataka viongozi wa wa ngazi zote za Chama  mkoani hapa kuwatembelea wanachama na kusikiliza kero zinazowakabili na kuhimiza umoja na mshikamano.

Katibu huyo  ambaye amehamia hivi karibuni mkoani Geita aliyasema haya juzi kwa nyakati tofauti alipofanya ziara ya kushtukiza katika baadhi ta matawi katika Kata ya Kalangalala ili kujua kama watandaji wa Chama wanatimiza majukumu yao.

Akiwa katika Tawi la Mbugani aliwaambia baadhi ya viongozi wa tawi hili aliowakuta aliwataka viongozi wote wa Chama kuanzia za matawi hadi ngazi ya mkoa kuhakikisha hawakai ofisini tu bila kuwatembelea wananchama kwa lengo la kukiimarisha Chama.

Alisema ili Chama kiwe imara kinapaswa kuwa na viongozi wanaojituma ,ambao wanasikiliza kero za wananchi na kuzifikisha kwenye mamlaka zinazohusika kwa ajili ya kutafutiwa ufumbuzi.

Aidha aliwataka viongozi hao kuhakikisha wanaweka mikakati ya ujenzi wa ofisi katika matawi ambayo hayana ofisi akisisitiza kuwa uimara wa Chama ni pamoja na kuwa na ofisi ambako wanachama na wananchi watafika kupeleka shida zao katika kuhamasisha hilo alichangia mifuko mitatu ya saruji katika tawi la mbugani.

Aidha aliwataka viongozi hao kufuatilia miradi mbalimbali inayotolewa pesa ili kujiridhisha kama inafanywa kwa ufanisi akiwataka kutoa taarifa kwake pale watakapohisi kuchezewa pesa ya serikali.




0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa