Home » » Mwanamke auawa katika fumanizi

Mwanamke auawa katika fumanizi



Na Faida Muyomba, Geita                 

MKAZI wa Kijiji cha Mwagimagi, Wilaya ya Geita, mkoani Geita, Bi. Dome Shaban (35), ameuawa kwa kupigwa na mumewe baada ya kumfumania akifanya mapenzi na mwanaume mwingine.

Akizungumza na waandishi wa habati, Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Leonard Paulo, alisema tukio hilo lilitokea Juni 11 mwaka huu, saa nane usiku na kumtaja mtuhumiwa wa mauaji hayo kuwa ni Bw. Faida Anthony (45), ambaye ni mume wa mwanamke huyo.


Alisema mwanamke huyo alifumaniwa akiwa na mwanaume mwingine ambaye jina lake halikufahamika wakifanya mapenzi chumbani wakati mumewe hayupo.

“Mtuhumiwa aliporudi nyumbani aligonga mlango na kukuta mkewe akifanya mapenzi na mwanaume mwingine ambaye alifanikiwa kukimbia na hadi sasa hajulikani jina lake na mahali anapoishi,” alisema Kamanda Paulo.

Aliongeza kuwa, mtuhumiwa alichukua kitu chenye ncha kali na kumchoma sehemu ya jicho la kulia la kushoto kabla ya kumpiga sehemu mbalimbali za mwili hadi kusababisha kifo chake.

Alisema mtuhumiwa alitoroka baada ya mauaji hayo ambapo Jeshi la Polisi linaendelea kumsaka.

Chanzo: Majira

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa