
Jumla ya Gramu 3263.72 za dhahabu zenye thamamani ya shilingi milioni 749,509,531.94 zimekamatwa zikisafirishwa kinyume cha sheria mkoani Geita.Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linawashikilia watu watatu waliokamatwa wakiwa na dhahabu hizo wakisafirisha kwa njia za magendo pia kinyume cha sheria kwa kutumia gari aina ya Toyota Premio yenye namba za usajili T.739 EEH mali ya Emanuel Kidenya Mkazi wa Kahama, Shinyanga.Waliokamatwa ni Yohana Idama (34), Mkazi ya Nyamhongolo wilaya ya Ilemela Mwanza, Moshi Manzili (26), Mkazi wa Bariadi Simiyu na Hamidu Salum (25), Mkazi wa Nyasubi wilaya ya Kahama Shinyanga.Watuhumiwa...