DHAHABU ZA MIL 700 ZAKAMATWA ZIKISAFIRISHWA KWA MAGENDO.

Jumla ya Gramu 3263.72 za dhahabu zenye thamamani ya shilingi milioni 749,509,531.94 zimekamatwa zikisafirishwa kinyume cha sheria mkoani Geita.Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linawashikilia watu watatu waliokamatwa wakiwa na dhahabu hizo wakisafirisha kwa njia za magendo pia kinyume cha sheria kwa kutumia gari aina ya Toyota Premio yenye namba za usajili T.739 EEH mali ya Emanuel Kidenya Mkazi wa Kahama, Shinyanga.Waliokamatwa ni Yohana Idama (34), Mkazi ya Nyamhongolo wilaya ya Ilemela Mwanza, Moshi Manzili (26), Mkazi wa Bariadi Simiyu na Hamidu Salum (25), Mkazi wa Nyasubi wilaya ya Kahama Shinyanga.Watuhumiwa...

RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKABIDHI TUZO KWA NSSF YA USIMAMIZI NA URATIBU WA HIFADHI YA JAMII KWA SEKTA BINAFSI NCHINI

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umeshinda tuzo ya Usimamizi na Uratibu wa Hifadhi ya Jamii kwa Sekta Binafsi  nchini, wakati wa kilele cha Maonesho ya Saba ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yaliyofanyika kwenye uwanja wa EPZ Bombambili, mkoani Geita. Tuzo hiyo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kupokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba wakati wa ufungaji wa maonesho hayo.Aidha, NSSF imeshinda tuzo ya mshindi wa kwanza katika kundi la Hifadhi ya Jamii na Huduma za Bima zilizotolewa Oktoba 12, 2024 na Mhe. Anthony Mavunde, Waziri wa Madini, wakati wa maonesho hayo.Akizungumza...

DC MASALLA ASHAURI MAONESHO YA NANENANE YAVUTIE ENEO LA MAZIWA MAKUU

Waandaaji wa maonesho ya Nanenane mikoa ya Kanda ya Ziwa Magharibi Mwanza,Geita na Kagera wameshauriwa kuzidi kuipa hamasha maonesho hayo na kuzifikia nchi zote za maziwa makuu kutokana na Mkoa wa Mwanza kuwa eneo la kimkakati.Rai hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masalla alipotembelea baadhi ya mabanda na kujionea na kupata taarifa mbalimbali kutoka kwa washiriki na kuhimiza fursa ya Mwanza kuwa eneo la kimkakati itumike vizuri kuyapa wigo maonesho hayo."Mwanza siku chache zijazo itazidi kuimarika hasa katika eneo la usafiri kuanzia wa anga,reli na barabara hivyo ni wakati mwafaka kwa waandaaji kuja na ubunifu wenye...

RAS GEITA AYAZINDUA RASMI MAONESHO YA NANENANE KANDA YA ZIWA MAGHARIBI.

Maonesho ya Nanenane 2024 Kanda ya Ziwa Magharibi yamezinduliwa rasmi leo Agosti 3,2024 kwenye viwanja vya Nyamhongolo huku yakionesha kuzidi kupata hamasa kutoka kwa wananchi.Akifungua maonesho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita,Katibu Tawala wa mkoa huo Mohamed Gombati amesema Jukwaa hilo liendelee kuwa somo kwa makundi mbalimbali yanayolengwa na maonesho hayo.Akiwa na mwenyeji wake Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Bw.Balandya Elikana,Gombati amatembelea mabanda mbalimbali na kujionea huduma zitolewazo na Taasisi,Halmashauri na makundi mbalimbali."Serikali ya Rais Samia ni kutaka Taifa lijitosheleze kwa chakula,uwekezaji katika kilimo na...

VICTORIOUS CENTRE CENTER OF EXCELLENCY WAWEKA MIKAKATI KUWASAIDIA WENYE USONJI

Na Mwandishi WetuKITUO cha Victorious Centre of Excellency nchini Tanzania kimesisitiza dhamira yake ya kujitolea katika kutoa matibabu ya uhuishaji na elimu kwa jamii kuhusu mahitaji maalumu kwa watoto wenye hali ya usonji hapa nchini.Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Victorious Centre of Excellency, Sarah Laiser-Sumaye ameelezea dhamira ya kituo hicho jijini Dar es Salaam hivi karibuni kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela yaliyoratibiwa na Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na Ubalozi wa Afrika Kusini nchini na kituo cha Victorious Centre of Excellence.Kupitia maadhimisho hayo wadau hao walifanya shughuli mbalimbali...

WANAFUNZI NAMNA PEKEE YA KUMLIPA RAIS SAMIA NI KUSOMA KWA BIDII-KATIMBA

Na Angela Msimbira, GEITANAIBU WAZIRI Ofisi ya Rais TAMISEMI (Elimu), Mhe. Zainab Katimba ametoa rai kwa wanafunzi wote nchini kuhakikisha wanasoma kwa bidii na kufaulu kwa viwango vya juu ili badae walitumikie taifa.Mhe.Katimba ametoa rai hiyo alipotembelea shule mpya maalum ya wasichana ya sayansi ya Mkoa wa Geita kwa lengo la kukagua miundombinu iliyojengwa na kujionea maboresho yaliyofanywa na serikali katika ujifunzaji na ufundishaji kwenye sekta ya elimu nchini.Amesema kuwa dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha watanzania wanapata elimu iliyobora katika mazingira mazuri hivyo ni wajibu wa wanafunzi...
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa