Home » » UFAHAMU MKOA WA GEITA KWA UPANA ZAIDI

UFAHAMU MKOA WA GEITA KWA UPANA ZAIDI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Meja Jenerali (Mst) Ezekiel E. Kyunga
Mkoa huu ulianzishwa mwaka 2012 kutoka  sehemu ya mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Kagera ukiundwa na Wilaya tano zenye Halmashuri Sita na majimbo saba (7) ya Uchaguzi. Mkoa una ukubwa wa eneo la km21,879 linalotumika katika shughuli za Kilimo cha mazao ya (Nanasi, Mahindi, Mpunga, Alizeti, Pamba na mazao mengine), Uchimbaji wa Madini aina ya Dhahabu katika Mgodi Mkubwa wa GGM na migodi midogo midogo, Biashara, Ufugaji, na uvuvi hususan maeneo ya Wilaya za Geita na Chato. Aidha Mkoa huu unasifika kuwa na hifadhi ya misitu mikubwa ya Kigosi /Moyowosi na kisiwa cha Rubondo kilicho ndani ya ziwa Victoria, kisiwa hiki kina wanyama adimu kama Statunga, Sokwe na eneo la mazalia ya samaki aina ya sangara.

Chanzo Tovuti ya Mkoa wa Geita 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa