Home » » MAKAMU WA RAIS MH.SAMIA SULUHU AANZA ZIARA MKOANI GEITA, AZINDUA MIRADI YA MAENDELEO

MAKAMU WA RAIS MH.SAMIA SULUHU AANZA ZIARA MKOANI GEITA, AZINDUA MIRADI YA MAENDELEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Mganga Mfawidhi wa Hospitali teule ya Mkoa wa Geita, Dkt. Adam Sijaona, wakati alipofanya ziara kwenye wadi ya wagonjwa wa upasuaji ya wanaume, katika Hospitali hiyo iliyojengwa kwa ufadhili wa Kampuni ya Geita Gold Mining (GGM). PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI, GEITA.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasalimia baadhi ya wananchi wa Mji wa Geita waliokuwepo Hospitalini hapo leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu (kulia) wakati wa ziara yake katika Hospitali teule ya Mkoa wa Geita, leo Januari 5, 2016. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mh. Fatma Mwassa pamoja na Mbunge wa Viti Maalum Geita Mjini, Mh. Vick Kamata.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea taarifa ya Hospitali teule ya Mkoa wa Geita, kutoka kwa Mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt. Joseph Kisala mara baada ya kuisoma. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mh. Fatma Mwassa. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na wananchi pamoja na wauguzi wa Hospitali teule ya Mkoa wa Geita. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea moja vifaa tiba vilivyokabidhiwa hospitalini hapo na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Geita Gold Mining (GGM), Terry Mulpeter, ikiwa ni sehemu ya mchango wao kwa jamii ya watu wa Geita, leo Januari 5, 2016. wengine pichani toka kulia ni Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mh. Suleiman Jaffo, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mh. Fatma Mwassa, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita, Dkt. Joseph Kisala, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu pamoja na Mganga Mfawidhi wa Hospitali teule ya Mkoa wa Geita, Dkt. Adam Sijaona.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akikabidhi vifaa hivyo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita, Dkt. Joseph Kisala, mara baada ya kukabidhiwa na Uongozi wa Kampuni ya Geita Gold Mining ambao wamekuwa ni wadau wakubwa wa maendeleo ya Mkoa wa Geita.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Geita Gold Mining (GGM), Terry Mulpeter, tuzo ya maalum ya kutambua Mchango wa Kampuni hiyo, kwa kujitoa kwake kuisaidia jamii ya watu wa Geita.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimtishwa ndoo ya maji, Bi. Tatu Salum, Mkazi wa kijiji cha Nyankubi Mkoani Geita, mara baada ya kuuzindua mradi mkubwa wa Maji Mkoani humo leo. Nyuma yake ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mh. Gerson Lwenge.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nyankubi Mkoani Geita, mara baada ya kuuzindua mradi mkubwa wa Maji Mkoani humo leo.

KUONA NA KUSOMA HABARI KAMILI BOFYA HAPA-MTAA KWA MTAA BLOG

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Geita Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa