Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mwenyekiti wa Jukata, Deus Kibamba,
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana mjini Dodoma na Mwenyekiti wa Jukata, Deus Kibamba, ilieleza kuwa Jukwaa hilo limeandika waraka kwenda kwa Mwenyekiti wa Bunge hilo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika kipindi cha kuahirishwa kwa Bunge hilo, serikali zote mbili ziendeshe zoezi la kupiga kura ya maoni ili wananchi wa pande zote mbili waamue juu ya aina ya Muungano wanaoutaka.
Alisema uchaguzi wa serikali za mitaa uliopaswa kufanyika Oktoba, mwaka huu, na ambao maandalizi yake hayajaanza kikamilifu uahirishwe na kufanyika pamoja na siku moja na uchaguzi wa mwaka 2015.
Alipendekeza Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutunga sheria itakayoweka ratiba mpya na ulazima kwa uongozi utakaochaguliwa mwaka 2015 kuendeleza mchakato wa katiba mara baada uchaguzi mkuu.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment