Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WILAYA ya Geita imebainika kuwa ni miongoni mwa maeneo ambayo
utumikishwaji wa watoto wadogo kwenye maeneo ya migodini unazidi
kushamiri.
Hayo yamebainika katika utafiti uliofanywa na shirika lisilo la
kiserikali la Nelico lililopo mjini Geita kwa kushirikiana na Shirika la
Codert na Plan International kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya.
Utafiti huo uliofanywa mwaka 2009, umebaini kuwa wanafunzi walioacha
shule na wale watoro sugu katika kata 11 za wilaya za Geita na
Nyangh’wale huku kukiwa na vijiji 51 na shule 65.
Ofisa Mradi katika mradi wa kuzuia ajira hatarishi kwa watoto hususan
migodini, Mbuya Viane, alisema baada ya kufanya utafiti huo wamegundua
ndani ya kata hizo 11 wanafunzi 12,300 wamepotelea katika shughuli za
migodini na uvuvi.
Mbuya alisema hadi sasa ni wanafunzi 5,191 tu ambao wamefanikiwa
kurudi shuleni tangu mwaka 2012 na 2013 huku akibainisha kuwa kati yao
2,231 walikuwa wameacha shule kabisa.
Alieleza kuwa watoro sugu ni 2,960, ambao ni wanafunzi kuanzia darasa la tatu hadi la saba.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment